Saturday, March 29, 2014

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete aiteka Kata ya Pera, Chalinze


1
Mgombea ubunge wa jimbo la Chalinze kupitia chama cha Mapinduzi Ndugu Ridhiwani Kikwete akiwahutubia wananchi katika viwanja vya kwa Mwarabu kata ya Pera Chalinze leo wakati wa mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo hilo, Unaotarajiwa kufanyika Aprili 6 mwaka huu jimboni humo, Ridhiwani amewaomba wananchi hao kumpa kura za ndiyo ifikapo Aprili 6 ili aweze kuwatumikia na kuleta maendeleo ya jimbo hilo akishirikiana na wananchi kwa ujumla wake uchaguzi huo unafanyika kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo marehemu Said Ramadhan Bwanamdogo.

2
Mgombea ubunge wa jimbo la Chalinze kupitia chama cha Mapinduzi Ndugu Ridhiwani Kikwete akipunga mkono juu huku Mzee Kazidi ambaye ni Katibu wa CCM mkoa wa Kilimanjaro na Meneja wa Kampeni wa mgombea huyo akicheza wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo kwenye Kata ya Pera. 3Imani Madega aliyekuwa mmmoja wa wagombea walioshiriki katika hatua za awali za mchujo ndani ya Chama cha Mapinduzi akimuombea kura Ridhiwani Kikwete wakati wa mkutano huo wa kampeni. 4
Mgombea ubunge wa jimbo la Chalinze kupitia chama cha Mapinduzi Ndugu Ridhiwani Kikwete na msafara wake wakiondoka katika kijiji cha Pingo Kata ya Pera mara baada ya kumaliza mkutano wa kampeni kijijini hapo. 5
Mgombea Ubunge wa jimbo la Chalinze kupitia chama cha Mapinduzi Ndugu Ridhiwani Kikwete akihutubia mkutano wa kampeni katika kijiji cha Pingo kata ya Pera leo. 7
Umati wa wananchi waliohudhuria katika mkutano uliofanyika kata ya Pera. 9Umati wa wananchi waliohudhuria katika mkutano uliofanyika kata ya Pera

No comments:

Post a Comment