Tuesday, August 5, 2014

MLEMAVU ATUMIA MGUU WAKE BANDIA KUFANYA BIASHARA HARAMU YA DAWA ZA KULEVYA


Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linamshikilia mlamavu aitwaye SAID S/O TINDWA, MIAKA 36, MKAZI WA VIJIBWENI  Wilaya ya Temeke kwa kosa la kufanya biashara ya dawa za kulevya.
 
Tarifa za kiintelijensia zilizopatikana kupitia kwa raia wema ziliwafikia makachero wa Polisi kuwa mlemavu huyo ambaye mguu wake wa kulia ni wa bandia amekuwa akiutumia vibaya mguu huo kwa kuficha dawa za kulevya ambazo aliwauzia watumiaji. Aidha kila kete alikuwa akiuza kwa shilingi Tsh.1000.


Ilikuwa mnamo tarehe 01/08/2014 katika mtego maalumu uliowekwa na askari wa upelelezi ndipo mlemavu huyo alikamatwa akiuza dawa hizo kwa wateja wake baada ya kuzitoa alikozificha ambapo ni ndani ya mguu huo wa bandia. 

Uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba mtuhumiwa huyo amekuwa akitumia mbinu hiyo kwa muda mrefu kabla ya kukamatwa. Aina ya dawa alizokuwa akiuza ni zile za viwandani kama vile Cocein , Heroin na wakati mwingine bhangi. Uchunguzi wa shauri hili bado unaendelea na jalada la kesi yake litapelekwa kwa mwanasheria wa serikali ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

Aidha natoa onyo kwa watu wenye ulemavu kwamba wasitumie kigezo cha ulemavu kufanya uhalifu kwa makusudi kwani wanawaharibia walemavu wengine ambao ni raia wema na ambao mara nyingi huonewa huruma na kutotiliwa mashaka.




S. H. KOVA,
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAAM

No comments:

Post a Comment