Friday, October 10, 2014

WANANCHI WASALIMISHA SMG MBILI KWA JESHI LA POLISI

kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Lineratus Sabas aakionyesho moja ya silaha ambazo zimesalimishwa  na wananchi


Jeshi la polisi mkoani Arusha limefanikiwa  kupata silaha mbili aina ya SMG ambazo  zilisalimishwa na wananchi katika mbili tofauti  huko wilayani ngorongoro.


Akiongea na waandishi wa habari kamanda wa polisi mkoani Arusha Lineratus Sabas  alisema kuwa Silaha hizo zilisalimishwa na wananchi katika siku tofa uti tofauti ambapo alisema kuwa silaha ya kwanza ilisalimishwa September 19   silaha aina ya SMG yenye NO.563651071iliopatikana katika eneo la harash ikiwa na risasi  mbili ndani ya magazine .

Alibainisha kuwa silaha ingine  ilisalimishwa September 26  ikiwa ni aina ya SMG yenye namba  ya usajili 514142 hii ilipatika katika eneo  ilo ilo la  la harash wilayani  Ngorongoro


Aliwapongeza wanachi kwa kutii sheria ya kusalimisha silaha hiiuku akitoa wito kwa wananachi wote popote pale walipo kusalimisha silaha ambazo wanahisi wanazitumia kinyume cha sheria.


Aidha alisema kuwa kama kuna mwananchi yeyote anaisi kuwa anamali nyingi na anaitaji kumiliki silaha basi afuate sheria zinazotakiwa .

No comments:

Post a Comment