Thursday, June 4, 2015

SEREKALI YAOMBWA KUPITIA UPYA SHERIA YA MTOTO YA MWAKA 1971 KWANI INAWAATHIRI WATOTO WENGI



mwenyekiti wa baraza la watoto wilaya ya Arusha Hassani Omary akizungumza wakati wa kongamano la  watoto ,walimu ,wazazi lililoandaliwa na shirikala intiative for youth (INFOY) kongamano lililofanyika ndani ya shule ya msingi ya uhuru jijini hapa



 baadhi ya wanafunzi ,wazazi na walimu waliouthuria katika kongamano hilo

mmoja wa mwanafunzi aliyeuthuria akieleza mathara ya mimba za utotoni
Na Woinde shizza,Arusha

 Serkali  imetakiwa kuangalia upya sheria ya  mtoto ya mwaka 1971

kwani ndio  imebainika kuwa ndio chanzo kimoja wapo kinachoruhusu na
kungangia ndoa za utotoni pamoja na mimba za utotoni.



Akizungumza wakati  katika wa kongamano lililoandaliwa na shirika la
intiative for youth (INFOY  )  mwenyekiti wa baraza la watoto wilaya
ya Arusha Hassani Omary amesema kuwa ni wajibu wa serekali kuangalia
upya sherika hii kwani sheria hii imekuwa ikiwaadhiri watoto wengi
hapa nchini.



Amesema kuwa sheria hii imekuwa ikiruhusu watoto hata wenye umri chini
ya miaka 18 kuolewa  iwapo tu wazazi wake watakapo kubali kitu ambacho
kinawaathiri watoto wengi katika masomo yao kwani wamekuwa
wanakatishwa masomo yao  na  iwapo akitokea mtu mmoja kupeleka lala
miko lake katika vyombo vya sheria amekuwa akishindwa kutokana na
sheria hii inaruhusu mtoto huyo ata awe mdogo kuolewa mradi tu familia
yake iwe imeafiki.



Aidha aliongeza  kuwa  mbali na sheria hii pia serekali ikinatakiwa
kutilia  mkazo sana katika mila mbalimbali na desturi zetu kwani mila
zingine zimekuwa zikichangia pia kwa kiasia kikubwa watoto wadogo
haswa wakike kukosa haki zao za msingi kwa kuwalazimisha kuolewa iwapo
tu viongozi wa mila zao wakitaka huku akitolea mfano kwa kwa kabala la
kimasai ambalo linaishi hapa Arusha na kudai kuwa wamekuwa wakisimamia
na kulazimisha watoto wao kuolewa pindi tu pale atakapo kuwa amevunja
ungo tu au pale atakapo uonekana amekuwa kidogo.



 Kwa upande wake Mratibu wa mradi wa  kulinda  na kutetea haya ya
sheria ya mtoto Laurent Sabuni alisema kuwa ni wajibu wa serekali
kutaangalia kwa makini sheria hii kwani imekuwa ikiweaathiri watoto
kwa kiasi kikubwa  kwa kuwakosesha haki zao .



Alisema kuwa  kumekuwepo na matatizo  ya watoto wadogo kupata mimba za
utotoni kutokana na pale wanapopeleka mashitaka katika vyombo vya
sheria  ,sheria hii imekuwa ikiwatetea wahalifu  hali ambayo imekuwa
ikiwapelekea watoto kukata hata tamaa ya kwenda kushitaki katika
vyombo vya sheria.



Kwa upande wake Afisa ustawi wa jamii  manispaa ya Arusha Saum Kweka
alisema kuwa  katika kipindi hichi ni wajibu wakila mzazi kuhakikisha
anamlinda mtoto wake anampa elimu mtoto wake kuhusiana na mimba za
utotoni .
Alisema kuwa kumekuwepo na watoto wengi wanapewa mimba wakiwa wadago
lakini kutokana na kutopata ushauri kutoelimishwa kutokaa karibu na
wazazi wao hivyo ni wajibu wa kila mzazi kuahakikisha anamuelimisha
mtoto wake kuhusiana na mazingira yanayomzunguka.



Aidha saum alisema kuwa ni wajibu wa kila mzazi kutambua kuwa
kumuozesha mtoto mdogo ni hatari na pia ni ukiukwaji wa sheria ,pia ni
kumkosesha haki za msingi mtoto hivyo ni wajibu wa kila mzazi kupiga
vita vikali  ndoa za utotoni pamoja na mimba za utotoni huku akigusia
kwa kusema kuwa kauli mbiu ya mwaka huu ni tokomeza mimba na ndoa za
utotoni sote kwa pamoja tunaweza.

Afisa ustawi wa jamii wa jiji la  Arusha Saum Kweka akichangia mada

No comments:

Post a Comment