Monday, June 13, 2016

WANANCHI WAJIPATIA PESA TASLIMU KWENYE MCHEZO WA SAKASAKA YA EFM REDIO



Mchezo wa SAKASAKA unaoendeshwa na kituo cha EFM redio umeanza rasmi siku ya jumapili ya Juni 12,2016 pale viwanja vya Mcanada, Tegeta ukiwahusisha wakazi wa wilaya ya Kinondoni. 

Kiasi cha shilingi milioni 3 taslimu zimetolewa kwa washindi 12 ambapo mshindi wa kwanza aliondoka na milioni mbili, wapili na watatu laki mbili, mshindi wanne hadi wasita laki moja na washindi sita wa mwisho kupata elfu hamsini kila mmoja.
Baadhi ya picha za washiliki wakisaka kitu kilichofichwa.
Umati wa watu waliohudhuria sakasaka katika viwanja vya Mcanada,Tegeta.
Mtangazaji wa Efm radio katika kipengele cha Fimbo chapa kinachosikika katika kipindi cha joto la asubuhi, Chogo akimuhoji mmoja wa washiriki wa mchezo huo.
Meneja matukio na mawasiliano Neema Godlays Mukurasi (kushoto) akimkabidhi mshindi mmojawapo wa sakasaka.
Mshindi wa kwanza Rashid Saleh Sengela (katikati) akisubili kupokea pesa yake baada ya kushinda shilingi milioni mbili taslimu.
Washiriki waliojipatia vitu vyao wakisubiria kuhakikiwa kama ni vya ushindi ama la ambapo miongoni mwao walijinyakulia pesa taslimu kutoka EFM radio.

No comments:

Post a Comment