Friday, September 23, 2016

waziri Kindamba Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu mpya TTCL


Rais Dkt. John Magufuli, amemteua Waziri Kindamba kuwa Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL.
Taarifa ya Ikulu jijini Dar es Salaam imesema uteuzi huo ni kufuatia hatua ya Serikali kununua hisa zote za Bharti Airtel ambaye alikuwa mbia mwenza wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) na hivyo Serikali kumiliki hisa za Kampuni hiyo kwa asilimia 100.
Kindamba ameteuliwa kushika nafasi hiyo kuanzia leo tarehe 23 Septemba, 2016.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo kufuatia uteuzi huo, aliyekuwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Dkt. Kamugisha Kazaura atapangiwa kazi nyingine.

No comments:

Post a Comment