Saturday, October 25, 2025

RAILA ODINGA JUNIOR AKABIDHIWA MIKOBA YA BABA YAKE

Kisumu, Kenya — 


Raila Odinga Junior ametambuliwa rasmi kama kiongozi mpya wa familia ya Jaramogi Oginga Odinga. Sherehe ya kitamaduni ya ‘liedo’, ikijumuisha nyimbo, ngoma za kienyeji na kunyoa nywele, ilifanyika nyumbani kwao Opoda kabla ya msafara kuelekea Kango ka Jaramogi.


Mheshimiwa Ruth Odinga, Mbunge wa Kaunti ya Kisumu (Woman Representative), alisema:


"Leo ni siku ya kumbukumbu na mwanzo mpya. Tunamuombea Junior hekima, ujasiri na uthabiti katika jukumu hili la kifamilia."


Tukio hili linathibitisha mwendelezo wa kizazi na heshima ya urithi wa familia ya Odinga, ukiwa na mshikamano wa kifamilia na jamii




















 

Thursday, October 23, 2025

SOMA MAGAZETI YA LEO 24 OCTOBA 2025






















MKUU WA WILAYA ATEMBELEA SAVVY FM 105.3 ARUSHA


Kushoto ni mkuu wa wilaya ya Arusha Joseph Mkude na kulia ni meneja wa savvy fm Mr.Borry Mbaraka.



Arusha
 Mkuu wa wilaya ya Arusha Joseph mkude leo  ametembelea kituo cha redio cha Savvy fm 105.3 katika kuendeleza ushirikiano na vyombo vya habari ndani ya jiji la Arusha


Mkuu wa wilaya ameweza kuzungumza na wanachi mbali mbali wa kanda ya kaskazini na kuwasisitiza kuendelea kudumisha amani sambamba na kujitokoze kwenda kupiga kura tarehe 29 octoba 2025.


Friday, June 15, 2018

SHUKRANI NA KUSITISHA MATANGAZO NA MACHAPISHO YETU RASMI

G SAMBWETI


Kwanza uongozi mzima wa G SAMBWETI blog  unatoa shukrani za dhati kwa wale wote waliowahi kutembelea blog hii ambao ni  watu zaidi ya laki nane elfu thelathini mia  tatu na arobaini na tatu (833343) tangu ilipoanzishwa hapo mwaka 2011 hadi  leo 15/06/2018

hatuna budi kuwashukuru sana kwani nilipenda kuendelea kuwahabarisha bali sheria za TCRA zinanilazimu  kusitisha  uchapishaji  katika gazeti lenu hilipendwa la  G sambweti blog.

pia napenda kutoa shukrani kwa wale wote waliokuwa wakisiliza salvation radio tz online kuwa matangazo hayo kwa sasa yamesimama rasmi.

Tutaonana tena  na kurudi hewani Mungu akipenda
salvation radio


asanteni sana nini mimi Gasper sambweti
0755 656445

sambweti@gmail.com