Wednesday, June 6, 2012

WAADISHI WA HABARI WATAKAIWA KWENdA KUSOMA

 Muwezeshaji wa semina ya waandishi wa habari akiendelea kutoa mada
 waandishi wa habari wa mkoani Arusha wakiuthuria semina wakiwa na mkurugenzi mtenaji wa UTPC

mkurugenzi mtendaji wa UTPC Abubakari Karsan katikati akiwa anawaonyesha waandishi kijarida chahabari

Waandishi wa habari jijini Arusha wametakiwa kwenda mashuleni kuongeza elimu ili kuweza kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazo ikumba fani hii katika kipindi hiki pamoja nakijacho
Hayo yamebinishwa mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari jijini hapa(APC)Claud Gwandu wakati akizindua mafunzo ya siku nne ya waandishi wa habari yaliyoandaliwa nchama hicho kwa kushirikiana na UTPC yanayofanyika katika ukumbi wa Olasiti jijini Arusha.

Alisema kuwa ni wajibu wa kila mwandishi wa habari kwenda kuongeza elimu ili kuweza kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo kukabiliana na upinzani wa soko la pamoja ambao kutakuwa na wati wengi kutoka katika nchi mbalimbali wanaofanya kazi hii ya uwandishi wa habari.

Alibainisha kuwa wanahabari wengi wa mkoa wa arusha wamekuwa wanapuuza kwenda kusoma kitu ambacho ni kibaya zaidi kwani  katika kipindi tunachoelekea itafikia mahala watu wengi watashindwa kufanya kazi hii kutokana na kutokuwa na elimu ya kutosha.

Gwandu aliongeza kuwa waandishi wahabari wanafursa mbalimbali ambazo zinawadia wao wenyewe kwenda kusoma hivyo ni juhudi ya kila mmoja kujitaidi kwenda kuongeza elimu.

Alibainisha kuwa hivi sasa kuna vyuo mbalimbali akitolea mfano vyuo vikuu huria vya tanzania ivyo ni vizuri kila mwandishi akajiunga katika vyuo hivi kwani vyuo hivi havibaini mtu kwa sababu vinamsaidia mtu kusoma huku anafanya kazi.
"hivi karibuni nimeenda jijini dar es salaam kwakweli napenda kuwapongeza sana waandishi wa habari wa jijini humo kwani asilimia kubwa nimewakuta wengi wao kila mmoja anasema anasoma mungine ananiambia anasema anashahada mungine hiki kweli namefurahi na nawapongeza"alisema Gwandu
Aliwasihi waandishi wa habari wa mkoa wa Arusha kuiga wenzao wa jijini dar es salaam ili na nyie muweze kuendelea ukibainisha kuwa kwa bahati mbaya katika kipindi hichi  ambacho serekali ipo katika harakati ya kupeleka sera mpya ya habari ambayo wanampango wa kupeleka bungeni.
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa UTPC Abubakari Karsan alisema kuwa waandishi wa habari wanafursa mbalimbali za kupata elimu ikiwa ni pamoja na kuandaa miradi na kutafuta wafadhili ambao watawasaidia na mtaweza kupata fedha za kusomea.

Alisema kuwa ktika kipindi hichi tunachoelekea mbali na uwandishi kila mtu anatakiwa kuongeza elimu ili kuweza kujikwamua kimaisha kwani huku tunapoelekea kama unaelimu basi sio kitu na hauwezi kunufaika kwa kitu chochote maana wenye elimu ndio watakuwa wanafaidika na wale ambao hawana wabakia kuteseka tu.

No comments:

Post a Comment