Tuesday, August 28, 2012

Vurumai ya Polisi na wana CHADEMA mkoani Morogoro h


Daima panapotokea vurugu au vita wanao athirika zaidi ni akina mama na watoto, na hii ndio hali hali ilivyokuwa hii leo mjini Morogoro ambapo Mama na mtoto, uchungu wa mwana aujuae mzazi, hapo kila mtu aliweza namna ya kujisalimisha na moshi wa mabomu baada ya kupigwa.
Askari akikimbilia gari baada ya kuanza kwa ufyatuaji wa mabomu katika eneo hilo
Mkuu wa Operesheni Sangara-Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) BENSON KIGAIYA akiwa chini ya ulinzi wa Polisi wa FFU 5 huku qwengine wakinyatia kwa pembeni. Akiambulia makofi ya mgongo na makalio.
 Boda Boda akimpa maji mtoto wa kike ili aweze kunawe kupunguza moshi wa mabomu yaliyopigwa na askari wa FFU wakati wakitawanya wanachadema ili wasiandamane katika kituo cha mafuta cha BP Msamvu.
 Huyu naye alikuwa akitembea huku gari la FFU likiwa nyuma yake baada ya kupigwa kwa mabomu eneo hilo la Msamvu.
 Mmoja wa kiongozi wa Chadema akitiwa nguvuni wakati wa maandamano hayo yanaendelea wakati wakielekea katika uwanja wa shule ya Kiwanja cha Ndege.
Mkuu wa Operesheni Sangara-Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) BENSON KIGAIYA akiwa chini ya ulinzi wa gari la polisi mara baada ya kukamatwa wakati wa zoezi la kuwapokea viongozi wa juu wa chama hicho kushindikana katika eneo la Msamvu kwa ajili ya maandamano kuelekea kwenye mkutano wa hadhara wa Chadema shule ya msingi Uwanja wa Ndege mkoani Morogoro.
 Hawa liingia kwa namna yake huku wakiwa na bango wakiingia kwenye uwanja huo baada ya askari wa jeshi la polisi kufanikiwa kuvunja maandano kwa baadhi ya makundi ya wanachadema.
Mfuasi wa Chadema akiwa na bango wakati akiingia katika uwanja wa shule ya msingi Kiwanja cha Ndegea kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa hadhara wa M4C. SOURCE: http://jumamtanda.blogspot.com/

No comments:

Post a Comment