Tuesday, July 29, 2014

MITAMBO NA VING’ORA KATIKA TAWI LA STANBIC BANK KARIAKOO VYAWAKIMBIZA/KUWAKURUPUSHA MAJAMBAZI KABLA YA KUKAMILISHA DHAMIRA YA KUPORA FEDHA ZA BANK


Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limeanzisha msako mkali wa kuwatafuta majambazi watano ambao jana tarehe 27/7/2014 saa 8.00 mchana walifika katika benki ya Stanbic Tawi la Kariakoo lililoko mtaa wa Swahili.

  Watatu kati yao waliingia ndani ya benki hiyo wakiwa na mifuko mikubwa wakijifanya ni wateja waliopeleka fedha nyingi katika benki hiyo.  Watu hao watatu walipoingia ndani walianza kulazimisha kuvuka wigo wa wateja wa kawaida na kutaka kuingia kwa nguvu kwenda kupora fedha.  

Stanbic Bank ina mitambo ya aina mbali mbali ikiwa ni pamoja na  ving’ora vya tahadhari.   Ving’ora hivyo vilianza kulia kwa sauti kubwa nje na ndani ya benk hiyo hali iliyowatia kiwewe wahalifu hao.  Waliamua kurudi nje kwa kasi ambapo kulikuwa na gari aina ya Noah na pikipiki moja ambazo hazikusomeka namba kwa haraka na wakatoweka baada ya kufyatua risasi hewani na kuwatisha watu waliokuwa nje na ndani ya Benk. 

 Baada ya kuondoka majambazi hao iligundulika kwamba mmojawao alichota kwa mkono kiasi cha fedha ambazo mteja alizileta kwa madhumuni ya kuziweka katika Tawi hilo.  Baada ya kutoroka majambazi hao waliteIekeza mifuko mikubwa ambayo walitegemea kubebea fedha watakazopora katika benk hiyo ambayo imehifadhiwa kama kielelezo na ndani ya mifuko hiyo waliweka kokoto na uchafu mwingine kwa madhumuni ya kuwadanganya walinzi na watumishi wa benk kwamba walikuwa wamebeba fedha za kuweka benki.

Kutokana na tukio hili tunahimiza benki zote kuchukua tahadhari za kiusalama ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba wanaingia mkataba wa kulindwa na Jeshi la Polisi, kuweka vifaa mbali mbali vya ulinzi vikiwemo ving’ora (alarms), CCTV Camera na mashine za kugundua (metal detectors) mtu anapoingia na silaha au kitu kingine cha hatari kama visu, mitarimbo n.k.

No comments:

Post a Comment