Friday, October 21, 2016

Clinton na Trump wataniana kwenye dhifa New York



Hillary Clinton na Kadinali Tim Dolan na Donald Trump - 20 Oktoba 2016
Wagombea wakuu wa urais nchini Marekani Hillary Clinton na Donald Trump walirushiana vijembe kwa utani katika dhifa ya jioni iliyoandaliwa kuchangisha pesa za hisani.
Walishiriki kwenye dhifa hiyo siku moja baada ya kushambuliana vikali kwenye mdahalo wa mwisho wa runinga.
Bi Clinton alicheka sana Bw Trump alipomtania kuhusu hotuba za kulipwa na pia uchunguzi wa FBI kuhusu tuhuma kwamba alitumia barua pepe ya kibinafsi kwa shughuli rasmi.
Lakini Bw Trump alizomewa alipofanya mzaha kwamba mpinzani huyo wake huwachukia Wakatoliki.
Dhifa hiyo ya Wakfu wa Ukumbusho wa Alfred E Smith mjini New York hufanyika kila baada ya miaka minne na kuwashirikisha wagombea urais.
Kuna desturi kwamba wagombea husimama na kutaniana, lakini mwana huu imeandaliwa wakati kumekuwa na uhasama mkubwa sana kwenye kampeni.
Jumatano jioni mjini Las Vegas wakati wa mdahalo wa mwisho, Bw Trump alimweleza mpinzani wake wa chama cha Democtaric kama "mwanamke mbaya", na wote na kila mmoja alikuwa anamkatiza mwenzake akiongea wakati wa mdahalo huo.
Mwishowe, walikataa kupatiana mikono kuagana.
Bw Trump amembandika "Crooked Hillary" (Hillary Mwovu) na ametishia kumteua mwendesha mashtaka maalum wa kumshtaki na kuhakikisha amefungwa jela iwapo atashinda.
Bi Clinton naye amesema mpinzani huyo wake wa chama cha Republican anaendesha "kampeni ya chuki na kuwagawanya watu" na kwamba hafai kuwa rais wa Marekani.
Lakini kwenye dhifa hiyo ya New York, walionekana kuweka kando tofauti zao kwa muda. Waliketi wakikaribiana sana, wakitenganishwa tu na KadinaliTimothy Dolan.
Walipoingia na kuketi, hawakusalimiana wala kuangaliana kwa macho. Lakini Bw Trump aliposimama kuhutubu, alimgusa begani kwa urafiki.
Alitania kwamba hadhira hiyo ya watu 1,500, ndio mkusanyiko mkubwa zaidi wa watu aliohutubia kufikia sasa.
Na akimshambulia Bi Clinton kwa uhusiano wake na matajiri wa Wall Sreet, akasema litakuwa jambo la ajabu sana kwa Bi Clinton kuwa na viongozi wengi hivyo wa mashirika na kampuni na awe hajalipwa.
Lakini aliposema mpinzani wake ni mfisadi kiasi kwamba alitupwa kutoka tume ya Watergate, alizomewa.
Na alizomewa tena aliosema Bi Clinton amekuwa "akijifanya kwamba hawachukii Wakatoliki". Matukio hayo mawili yalionekana kumfanya Bi Clinton kutabasamu.
Hillary Clinton na Kadinali Tim Dolan na Donald Trump - 20 Oktoba 2016Image copyrightAFP
Image captionWalitaniana ingawa wakati mwingine walirushiana vijembe
Bw Trump pia alijitania kwa kugusia hotuba ya mkewe Melania aliyoitoa Julai, ambapo alidaiwa kukopa sana maneno kutoka kwa Mama Taifa Michelle Obama.
Kisha, Bi Clinton alisimama kuhutubu. "Tutakuwa na mwanamke wa kwanza rais au rais wa kwanza aliyeanzisha vita kwenye Twitter na Cher," alisema.
Badala ya kutazama Sanamu ya Liberty kama mnara wa matumaini, Bw Trump amekuwa akigeza urembo wa sanamu hiyo. Alama "nne" au "tano labda" iwapo sanamu hiyo itapoteza mnara wake na tablet na kubadilisha nywele, Bi Clinton alitania. (Bw Trump wakati aliendesha shindano la urembo na ametuhumiwa kuwadhalilisha wanawake).

No comments:

Post a Comment