Saturday, October 22, 2016

SHIRIKA LA IDADI YA WATU DUNIANI (UNFPA) LAZINDUA TAARIFA YA HALI YA IDADI YA WATU DUNIANI


wez1
Mgeni Rasmi Mhe. Mahmoud Thabit Kombo, Waziri wa Afya, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar  (mwenye kaunda suti ya kijivu) akiwa katika Jukwaa Kuu na viongozi waandamizi kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na viongozi kutoka Shirika la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA).  Wengine pamoja nae ni Bw. Barnabas Yisa, Ofisa Mkaazi Mfawidhi UNFPA Tanzania (kushoto) na Mhe. Issa Juma Ally, Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B (kulia).
wez2
Mhe. Salama Abuu Talib, Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira ambaye pia ni Kaimu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango, Zanzibar akihutubia wananchi waliohudhuria sherehe hizo.
wez3
Wananchi wa kijiji cha Kilombero, Wilaya ya Kaskazini B, Mkoa wa Kaskazini Unguja wakifuatilia kwa makini yaliyokua yakijiri wakati hafla ya uzinduzi wa taarifa hiyo.  
wez4
Bw. Barnabas Yisa, Ofisa Mkaazi Mfawidhi UNFPA (mwenye shati jeupe) akitoa neno kwa wananchi walioshiriki shughuli ya uzinduzi wa Taarifa ya Hali ya Idadi ya Watu Duniani. Kushoto ni Bibi. Christina Mwanukuzi Kwayu, Mwakilishi Msaidizi, UNFPA akitafsiri kwa lugha ya kiswahili hotuba ya Ofisa Mkaazi Mfawidhi.
wez5
Mhe. Issa Juma Ally, Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B, akitoa neno kwa wananchi waliohudhuria uzinduzi wa Taarifa hiyo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi ili aweze kuongea na wananchi na kuizindua rasmi.
wez6
Mgeni Rasmi Mhe. Thabit Kombo, Waziri wa Afya, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar akieleza juu ya fursa ndogo waliyonayo wasichana ya kumaliza skuli kuliko wavulana na wako katika hatari zaidi ya kukabiliwa na ndoa za utotoni, ajira za watoto, ukeketaji na matendo mengine ya udhalilishaji.
wez7
Mhe. Thabit Kombo, Waziri wa Afya, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Taarifa ya Hali ya Idadi ya Watu Duniani.
wez8

Mgeni Rasmi Mhe. Thabit Kombo, Waziri wa Afya, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar akiwaonyesha wananchi kitabu cha Taarifa ya Hali ya Idadi ya Watu Duniani mara baada ya kuizindua.

No comments:

Post a Comment