Thursday, June 8, 2017

Uchaguzi mkuu Uingereza: Wapiga kura kuingia vituoni leo

Polling stationHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionKituo cha kupigia kura
Mamilioni ya watu leo watapiga kura kwenye uchaguzi mkuunchini Uingereza.
Shughuli ya upiganji kura itaaza mwendo wa saa moja asubuhii saa za Uingereza wakati zaidi ya vituo 40,000 vitafunguliwa kote nchini.
Jumla ya wabunge 650 watachaguliwa huku takriban watu milioni 46.9 wakiwa wamejiandikisa kupiga kura.
Ni ongezekao kutoka uchaguzi wa mwaka 2015 wakati wapiga kura milioni 46.4 walikuwa wamejiandikisha.
Kura zingine tayari zimepigwa kupitia kwa posta ambayo ilichukua asilimia 16.4 wakati wa uchaguzi wa mwaka 2015.
Vituo vingi vya kupigia kura viko shuelni na katika vituo vya kijamii.
Matokeo ya viti kadha yanatarajiwa kutangazwa ifikapo usiku wa manane huku matokeo ya mwisho yakitarajiwa kutangazwa ifikapo Ijumaa mchana.
David DimblebyHaki miliki ya pichaJEFF OVERS
Image captionDavid Dimbleby ataongoza matangazo ya runinga BBC

No comments:

Post a Comment