Monday, June 11, 2012

BAKWATA YATOA TAMKO

BARAZA kuu la waislam nchini, BAKWATA, Mkoa wa Arusha, limemtaka Askofu  wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri  KKKT Dayosisi ya mkoani Arusha,Thomas Lazier,  kuthibitisha madai yake aliyoyatoa hivi karibuni katika Vyombo vya habari  ya kuwepo Vijana zaidi ya 300 wanaofanya mazoezi kwa ajili ya kuchoma makanisa na kuharibu mali mbalimbali zinazomilikiwa na makanisa  mkoani Arusha vinginevyo Bakwata, itachukua hatua zinazostahili dhidi ya madai hayo.

Kauli hiyo imetolewa  na Shekh, wa Bakwata Mkoa wa Arusha, Shaaba Juma,alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari  kufuatia taarifa zilizoandikwa katika  vyombo vya habari hivi karibuni zikimnukuu AskofuThomas Laizer, wa KKKT,  akiwatuhumu Vijana zaidi ya 300, wa kiislam kuwa wanakusanyika kila siku na  kufanya mazoezi ya Karate,kwa kujiandaa kuchoma na kuharibu  makanisa mkoani Arusha.

Shekh, Shaaban amesema Bakwata imeshitushwa na taarifa hizo za kuwepo kundi laVijana 300 wa kiislam,wanaofanya mazoezi ya Karate, katika msikiti ambao hakuutaja jina lake aliodai kuwa upo katika   Eneo la  Unga limited jijini Arusha, wanaofanya mazoezi kwa ajili ya  kuchoma makanisa na kuharibi  mali mbaklimbali zinazomilikiwa na makanisa..

Alisema kuwa mara baada ya kupata taarifa hiyo ya kusikitisha, aliitisha kikao  na Mashekh , Maimam na walimu wa madrasa katika kata ya Unga limited ambapo viongozi hao walisikitishwa na taarifa hiyo ambayo walisema haina ukweli wowote na kama Askofu huyo anao ushahidi wakamtaka   kutoa taarifa hiyo kwenye vyombo vya Ulinzi na Usalama ili ifanyiwe kazi.

Shekh Shaaban, alisema kuwa amewasiliana na mkuu wa mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, ambae wamekubaliana  kukutana siku ya  Jumatano  Julai 13 mwaka huu  ili Askofu, huyo aweze kutoa ufafanuzi wa madai yake hayo mbele ya viongozi wa Dini na Serikali ili kupata  ukweli wa madai hayo .

“Mimi  Shekh  wa mkoa sina taarifa hizo ninaona taarifa hii ni ya hatari, inayolenga kuchafua Uislam na Waisam, nimefuatilia  sijaona ukweli wowote kuhusu madai hayo,   Kauli ya  Askofu haifai kupuuzwa hata kidogo kwa sababu imetolewa na kiongozi mkubwa wa Kanisa” alisema Shehk shaaban
.
Shekh, shaaban, alisisitiza kwamba  hakuna msikiti wenye Vijana 300 kama inavyodaiwa na Askofu huyo, wanaofanya mazoezi  ya Karate,kwa ajili ya kuyachoma moto makanisa,na kufanya uharibifu wa mali  kauli hiyo inalenga kuchonganisha Waislam na Wakiristo na serikali yao na hivyo kujenga Taswira mbaya  dhidi ya Dini Kiislam .

Akasisitiza kuwa Waislam na wasiokuwa waislam siku zote wameishi kama ndugu hivyo kauli hiyo isitumike kujenga   fitina ya  kuwagombanisha wananchi na kuvuruga amani na utulivu uliopo hapa nchini ambao umedumu kwa miaka mingi kwa kutambua kuwa kila mmoja ana uhuru wa kuabudu dini aitakayo.hivyo kama anazo taarifa sahihi aziwasilishe kwenye vyombo vya dola alisisitiza shehkh Shaaban.

Hivi karibuni magazeti ya Habari leo la juni 4 na An –Nuur ya Ijumaa Juni  8 yenye vichwa vya habari tofauti yalimnukuu Askofu Laizer,ambapo gazeti la Habari leo liliandika Uamsho waibukia Dar es Salaam, wakati gazeti la An –Nuur ,likiandika Askofu Laizer, anawajua waliochoma moto  makanisa hata hivyo    baadhi ya viongozi wa makanisa wakiwemo mapadri, wamesema  madai ya Askofu huyo yatapelekea   kuwachonganisha waislam na dini zingne i kwa kuwa hakuifanyia utafiti  

No comments:

Post a Comment