Monday, June 11, 2012

SHULE AMBAZO HAZITAKUWA NA MATOKEO YA UHAKIKA ZITAFUTIWA USAJILI

AFISA kwa shule za msingi katika Halmashauri ya Manispaa ya Arusha Bw Omary Mkombole amesema kuwa katika msimu wa Mithiani ya mwaka 2012 shule yeyote ambayo itaonekana kuwa na kasoro za majibu ya mithiani basi atalazimika kushinikiza shule hizo zifutiwe usajili wa kudumu
 
Alitoa Kauli hiyo mjini Arusha wakati akifungua mkutano baina ya wamiliki na mameneja wa shule binafsi kwa mkoa wa Arusha (TAMONGSCO)mapema wiki iliyopita.
 
 Mkombole alisema kuwa haina tija kabisa kwa Shule ambazo zinadanganya matokeo kuendelea kuwepo kwa kuwa  hali hiyo ndiyo inayochangia kwa kiwango kikubwa sana kuongeza hata idadi ya wasiojua kusoma na kuandika ndani ya Taifa.
 
Alisema kuwa kamwe ndani ya mwaka huu wa 2012 hatakubali kuona hali hiyo inajitokeza kama ilivyojitokeza kwa mwaka 2011 na badala yake shule ambayo itajitokeza na hali hiyo ni lazima ichukuliwe sheria kali kabisa.
 
“leo mpo hapa wamiliki na mameneja wa shule kama mnataka kushika nafasi za kwanza hakikisheni kuwa mnawafundisha watoto wenu kwa bidii na wala sio kuwapa majibu na shule yeyote itakayofanya hivyo mwaka huu nilazima ifutiwe usajili kwa kuwa wanaopata shida ni hawa wanafunzi”alisema bw Mkombole.
 
Awali aliwataka wamiliki wa shule pamoja na Mameneja wa shule binafsi kuhakikisha kuwa wanajijengea tabia ya kuajiri walimu wenye sifa kwa kuwa walio ambao hawana sifa ndio chanzo pekee cha kuwapa watoto mbinu za udanganyifu ili waonekane kama wamefanya vema kumbe wamedanganya Jamuhuri.
 
Mkombole alisema kuwa ili shule iweze kushika nafasi za kwanza zinatakiwa kuwa na walimu wenye ubora ambao unaitajika kwa kiwango cha hali ya juu ambapo kwa kufanya hivyo pia wataimarisha hata uchumi wa nchi
 
Katika hatua  nyingine Mwenyekiti wa chama hicho cha wamiliki wa shule binafsi kwa mkoa wa Arusha  Ester Lema alisema kuwa pamoja na kuwa shule hizo zimekuwa ni msaada mkubwa sana kwa mkoa wa Arusha lakini bado zinakabiliwa na changamoto kubwa sana .
 
 Lema alitaja changamoto kubwa  ambayo kwa sasa wanakabiliwa nayo ni pamoja na changamoto ya ulipaji wa kodi kubwa sana huku nao wakiwa wanachangia kusaidia Serikali kuhusiana na kuwaelimisha watoto wa Kitanzania,
 
Aliitaka Serikali kuweza kuangalia tena mchakato wa kodi kubwa sana hasa kwa shule binafsi kwa kuwa changamoto hiyo nayo imekuwa ni mzigo mkubwa sana kwa wamiliki na hata Mameneja wa shule binafsi.
 

No comments:

Post a Comment