BARAZA
la Habari nchini ( MCT ) limewataka wahariri wa vyombo vya habari
nchini kushirikiana kikamilifu na MCT ikiwa ni pamoja na kutoa maoni
mbalimbali badala ya kujitenga kama ilivyo sasa.
Katibu Mkuu wa
MCT, Kajubi Mukajanga alisema hayo jana alipozungumza katika mkutano wa
kwanza wa mwaka wa mashauriano baina ya wahariri na MCT uliofanyika
mjini Morogoro ambao unaojadili kuimarisha weledi na uwajibikaji wa
taaluma ya habari nchini.
Alisema wahariri ni miongoni mwa
wanachama wa MCT kupitia vyombo vyao vya habari ambapo alisema kuwa
kinachoshangaza ni kuona wahariri hao wanajitenga na baraza hata katika
kusukuma ajenda mbalimbali na hivyo kuviachia vyama vya waandishi wa
habari wa mikoani kuwa na nguvu ya kusukuma ajenda zao.
“Wahariri
ni wenye uwezo mkubwa wa kufanya uamuzi mbalimbali katika vyombo vyao
ikiwamo kuruhusu habari ziingie na kutoka na hivyo wana uelewa na ndio
wanaoowaongoza waandishi wao hivyo wao ndio walitakiwa kuwa na nguvu
kubwa ya kusukuma ajenda za MCT,” alisema.
Aidha aliwasisitiza
wahariri hao kuchukua nafasi zao kama wanachama wa MCT katika kutoa
maoni na ili itende kwa matakwa vyombo vya habari wanavyotoka.
Alisema
kuwa MCL imekuwa ikifanya shughuli zake za kusuluhisha migogoro
mbalimbali ikiwamo ya wahariri na waandishi wa habari na hata wadau na
waandishi au vyombo vya habari na wanachama wamekuwa wakinufaika kupitia
usuluhishi huo badala ya watu kukimbilia mahakamani ambako mara nyingi
huishia pabaya.
Hata hivyo alisema kuwa kamati ya maadili ya MCT
imekuwa ikitekeleza shughuli zake kwa asilimia 90 hali ambayo ni ya
kujivunia katika tasnia ya habari na hivyo wahariri wamekuwa
wakikubaliana na uamuzi wa MCT. |
No comments:
Post a Comment