Maandamano ya Waislamu yameenea sehemu nyingi duniani wakipinga
filamu iliyotengenezwa Marekani na inayomkashifu Mtume Muhammad, ambapo
polisi wa Cairo wametumia mabomu ya machozi kutawanya waandamanaji hao.
Wizara ya afya ya Misri imesema watu kumi na tatu wamejeruhiwa katika maandamano hayo ambapo waandamanaji wameshusha bendera ya Marekani na kuichoma na kisha kupandisha bendera nyeusi.
Serikali ya Misri imetoa wito kwa raia wake kurejesha amani huku pia ikiikosoa filamu hiyo ambayo imeleta hasira nchini Libya na kusababisha vifo vya raia wanne wa Marekani akiwemo Balozi Chris Stevens mjini Benghazi.
Katika taarifa ya baraza la mawaziri iliosomwa na Waziri Mkuu Hisham Qandil , uongozi wa nchi hiyo umesema filamu hiyo imemdhalilisha Mtume Muhammad na pia imekiuka maadili. "Tunawaomba wananchi wote wa Misri kueleza hasira zao kwa amani," imeeleza sehemu ya tamko hilo.
No comments:
Post a Comment