Wednesday, March 13, 2013

Karinali Jorge Mario Bergoglio toka Argentina ateuliwa kuwa Papa mpya


new popeMaelfu ya waumini waliokuwa wamekusanyika katika viunga vya Kanisa la Mtakatifu Peter Basilica, walipiga kelele za furaha zilizoambatana na dua za kumshukuru Mungu, baada ya kuona moshi mweupe ukianza kusambaa katika anga la eneo hilo toka katika jumba ambako Makadinali 115 walikuwa wamejifungia kwa ajili ya kuendesha zoezi la kumchagua kiongozi mkuu mpya wa Kanira Katoliki duniani.

Na kelele hizo ziliongezeka maradufu zikiambatana na vigelegele vya shangwe na nderemo, pale Karinali Jorge Mario Bergoglio, raia wa Argentina mwenye umri wa miaka 76, alipojitokeza katika lango kuu la nyumba walikokuwa wamejifungia, huku akipunga mikono ya furaha yenye kuashiria mwanga mpya kwa waumini wa kanisa katoli kote duniani.

Kuna mambo mawili ambayo yameleta msisimko mkubwa katika uteuzi huu. La kwanza likiwa ni lile la Waitaliano ambao walikuwa na matumaini makubwa ya kurejea katika kushikilia wadhifa huo kuukosa tena kwa mara ya tatu, na la pili likiwa ni ukweli kuwa, hii ni kwa mara ya kwanza kwa Papa kutoka katika nchi zinazoitwa za ulimwengu wa tatu.

Karinali Jorge Mario Bergoglio, amechagua kuwa aitwe Papa Francis wa kwanza.

No comments:

Post a Comment