Wednesday, May 1, 2013

WAFANYAKAZI 24 WAPATA ZAWADI ZA WAFANYAKAZI BORA LEO KATIKA MAADHIMISHO YA MEI MOSI JIJINI DAR ES SALAAM




 Baadhi ya wafanyakazi kutoka Wizara mbalimbali za Serikali na Taasisi Binafsi wakiwa katika foleni wakijiandaa kuanza maandamano kuelekea kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja kwa ajili ya kushiriki maadhimisho ya Sherehe za Mei Mosi, ambapo katika Sherehe hizo mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Saidick, huku sherehe hizo kitaifa zikifanyika Kitaifa Mkoani Mbeya, na Mgeni Rasmi huko ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.

Mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick, akiwa meza kuu na baadhi ya viongozi wengine wakati wakisimama kupokea maandamano hayo.
 Wafanyakazi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii NSSF, wakipita mbele ya jukwaa kuu na maandamano na mbwembwe za kucheza Kiduku, wakati wa sherehe hizo.
 Wafanyakazi wa TALGWU, wakipita mbele ya jukwaa kuu na Bango lenye ujumbe.
 Twiga Cement wao walikuwa wakipromoti bidhaa yao tu bila hata bango lenye ujumbe kuhusiana na sherehe hizo.
 Maandamano yakiendelea kupita mbele ya jukwaa kuu.
 Maandamano yakipita mbele ya jukwaa kuu........
 'Watenda Haki' wakipita na bango lao mbele ya jukwaa kuu......SOURCE:SUFIANMAFOTO BLOG

habari na mhariri mkuu wa G SAMBWETI

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh Sadik Meck  Sadik amewaongoza leo wafanyakazi wa vyama mbali mbali vya jiji la Dar es salaam katika kuadhimisha siku ya wafanyakazi duniani na kauli mbiu ha mwaka huu ikiwa ni KATIBA MPYA IZINGATIE USAWA NA HAKI KWA TABAKA LA WAFANYAKAZI; na wafanyakazi wapatao 24 walitunukiwa zawadi za ufanakazi bora mwaka huu. 

Maadhimisho ya siku ya wafanyakazi kwa jiji la Dar es salaam yamefanyika katika viwanja vya mnazi mmoji huku kitaifa ikifanyik mkoani mbeya na mgeni rasmi akiwa ni rais wa jamhuri yaMuungano dk Jakaya Mrisho  kikwete.

katika siku ya leo wafanyakazi kutoka vyama mbali mbali wameitikia wito wa kuhudhuria na  kusababisha uwanja wa mnazi mmoja kufurika  watu  na kusababisha  magari kutoka makampuni mbali mbali kukosa sehemu ya maegesho ya kuonyesha kazi zao .

Katika  risala iliyosomwa mbele ya mgeni rasmi mh Sadik meck sadik , kuliorodheshwa changamoto mbali mbali zinazowakabili wafanyakazi mojawapo likiwa ni tatizo la ongezeko la nauli,tatizo la makato  kutofautiana baina ya vyama na vyama,tatizo la kuchelewa kupelekwa kwa makato ya mfanyakazi.

Mwisho risali ilimaliziwa kwa kutoa ombi kwa serikali kukomesha tabia ya  waajiri wa sekta binafsi kuwafanyisha kazi kwa muda mrefu wazawa huko wafanyaka kutoka nje wakifanya kazi  ambazo ni za muda mfupi kwa mishahara minono ,kazi ambaZo hata watanzania wanaziweza.

Nae Mgeni rasmi   katika kujibu risala hiyo ya wafanyakazi amewahakikishia kuwa mwakani watatumia uwanja wa uhuru ili kuepuka msongamano , pia aliweza kuongelea na kuwahoji wakuu wa wilaya kuhusu tatizo la kuchelewa kupelekwa kwa makato ya wafanyakazi katika  mifuko ya pensheni na kuweka tamko kuwa ifikapo juni 30 makato ya wafanyakazi wote yawe yamepekwa katika mifuko husika ya pensheni.

Na katika suala la kupunguza matatizo ya msongamano mh Sadik amesema kuwa  hadi kufikia mwezi wa nane mwaka huu watazindua usafiri wa majini kwa kutumia boti kutoka kivukoni hadi bagamoyo  ambapo boti hiyo itasimama katika vituo vinane  pia akagusia  matarajia ya mabasi makubwa ili kupunguza na kutokomeza suala la foleni na pia kutokomeza tatizo la usafiri ,huku akiwatoa hofu wamiliki wa daladala kuwa watapa vibali vya kufanya kazi katika mikoa mingine yenye uhitaji wa daladala na mwisho kabisa mgeni rasmi aliwakimbusha wafanyakaji kukumbuka kujikinga na gonjwa hatari la ukimwi. 

No comments:

Post a Comment