Tuesday, June 25, 2013

G-Nako sasa katika Kandanda?


G Wara wara toka Crew la Nako2Nako na kampuni ya WEUSI anakuja na SNIPPET yaani KIONJO tu cha wimbo wake mpya utakaoingia sokoni hivi karibuni ikiwa ni mkono toka Noizmekah production studios kwa Defxtro, Snippet hii ni ya wimbo wa " Wara na Mpirahttp://www.hulkshare.com/rqfljqaby2v4" alomshirikisha Mkali wa RnB BenPol,Sasa hatuelewi Soka na Muziki kwa namna gani vinahusiana hapa ila tumuachie Fanani Gnako atupe ladha kidogo then baadae tutaelewa zaidi, Kwa sasa pata kionjo HAPA na endelea kusupport Muziki wa Tanzania, kwa mawasiliano na mahojiano zaidi check na Gnako mwenyewe kupitia Facebook hapa na kikubwa zaidi ni maboresho ya Muziki na maisha yetu wasanii wa Tanzania, "Kwa mara nyingine nitoe pole kwa familia zote zilizopatwa Misiba ya wasanii wenzetu,Mangwea, Sharo, Langa na nitoe wito kwa wapenzi wa Muziki wa Bongo wasisite kutuunga mkono kwa hali na mali, ningependa kuweka wazi kwa mashabiki wote kuwa wimbo wangu huu "Wara na Mpira" Nitauweka sokoni kwa mauzo kupitia nambari za simu nitakazozitaja hapo baadae ili True fans wangu waweze kuupata wimbo kamili kabla haijasambazwa katika media Yoyote..One loveWaraBenPol_500.png

No comments:

Post a Comment