Sunday, July 7, 2013

BREAK NEWS WATU WATANO WAFARIKI HUKO MIRERANI BAADA YA KUANGUKIWA NA NGEMA

Habari kutoka mji mdogo wa mirerani  mkoani manyara zinasema watu watano wamepoteza maisha katika machimbo ya  madini aina ya Tanzanite , yaliyotokea jana usiku katika  mdogo wa block D.

Akiongea na radio five Arusha leo asubuhi shuhuda wa tukio hilo amesema mgodi huo ambao mmiliki wake ametambulika kwa jina la  bwana Onesmo   limeua baada ya kuanguka kwa ngema  katika mgodi huo.

chanzo cha kuanguka kwa  ngema hiyo ni baruti ambayo ililipuliwa katika mgodi huo na kwa bahati mbaya ngema ikadondoka na kuua watu wachimbaji wawili baada ya kufunikwa kwa ngema au kifusi cha majabali makubwa .

Baada ya kutokea kwa tukio hilo na watu wawili kupoteza maisha majira ya saa mbili   ,waokoaji watatu walikwenda ili kuwakuwasaidia lakini ilipofika majira ya saa tatu usiki ikagundulika kuwa nao wamepoteza maisha  katika shimo la mgodi huo.


Juhidi za kuopoa miili ya marehemu imeshamilika na taratibu za kupeleka miili hiyo katika hospitali ya mkoa ya mount Meru imefanyika ili kuhifadhi  miili hiyo  na walitambulika  katika tukio hilo ni fundi Kavishe,God, Ndianka na Ndekira na kwamba shuhuda wa tukio hilo alikuwa anahabarisha habari moja kwa moja kutoka katika sehemu ulipo msiba wa marehemu Ndiaka

blog hii inatoa pole kwa wale walifikwa na  msiba huu Mungu ametoa na Mungu ametwaa jina lake lihimidiwe na roho za marehemu zipumzike kwa Amani.

No comments:

Post a Comment