Thursday, February 20, 2014

PSPF YATOA ELIMU YA MFUKO WAKE KWA WANAHABARI NA WADAU WA MFUKO HUO LEO JIJINI DAR ES SALAAM

1Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa PSPF Bw. Adam Mayingu akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wadau wa mfuko huo katika semina iliyoshirikisha waandishi wa habari pamoja na baadhi ya wadau wa mfuko huo kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na mfuko huo na fursa mbalimbali pamoja na mafao mbalimbali yanayotolewa na mfuko huo ambapo wakuu wa vitengo mbalimbali wameelezea jinsi mfuko huo unavyofanya kazi zake na ukusanyaji wa michango ya wanachama, Mfuko huo umewaasa waandishi wa habari kujiunga na mpango wa hiari ambao una faida kubwa sana kwa mwanachama atakayejiunga na PSPF, Semina hiyo imefanyika katika ukumbi wa JB Belmont Hotel jengo la Golden Jubilee Towers jijini Dar es salaam.1aMamaa Thauda wa Nguvu kutoka Chanel 5/ EATV ameshiriki katika semina hiyo hapa akisikiliza mambo muhimu yaliyokuwa yakielezwa katika semina hiyo 2Neema Muro Mkurugenzi wa Uwekezaji katika mfuko huo akitoa mada juu ya uwekezaji katika mfuko wa PSPF. 3Mkurugenzi wa Fedha Masha Mushomba akizungumzia masuala ya fedha na ukusanyaji pamoja na ulipaji mafao kwa wanachama wa mfuko huo. 4Andrew Nkangaa Mkurugenzi wa Tehama katika mfuko huo akizungumzia jinsi wanachama wanavyoweza kuchangia mfuko huo kwa kutumia mitandao ya simu na  kurahisisha shughuli zao za kila siku badala ya kufuata ofisi za PSPF zilipo kwa ajili ya kwasilisha michango yao. 5Mkurugenzi wa mtandao wa www.fullshangweblog.com Bw. John Bukuku kulia akiwa na Mkurugenzi wa 8020fashion Shamimu Mwasha katika semina hiyo

No comments:

Post a Comment