Thursday, June 12, 2014

UJANGILI :JESHI LA POLISI DAR ES SALAAM LAKAMATA VIPANDE 54 VYA MENO YA TEMBO

Displaying DSC03492.JPGJeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaa limefanikiwa kuwakamata watu  watatu kwa tuhuma za kupatikana na vipande 26 vya meno ya Tembo kinyume cha sheria. Tukio hili lilitokea  tarehe 29.05.2014 huko maeneo ya M’nyamala Kata ya Mwinyijuma Osterbay (M) Kinondoni

baada ya  jeshi la polisi kupata taarifa toka kwa msiri, kuwa kuna gari namba  T 178 BSY aina NOAH inasemekana ina mizigo ya wizi.  Baada ya taarifa hizo askari walijipanga na kuweka mtego, na kufanikiwa kulikamata   hilo , na walipolipekuwa walikuta viroba viwili ,vilivyokuwa na vipande hivyo vya meno ya tembo ambavyo thamani yake haikufahamika mara moja. Watuhumiwa pamoja na gari husika wanashikiliwa na  Watuhumiwa hao ni kama ifuatavyo:
·       ADAM  YONA, miaka 37,  mkazi wa Mbagala,
·       SELEMANI  LEONALD, Miaka 37, Mkazi wa M’nyamala,
·       HUSSEIN  SAID, Miaka 34,
Katika tukio la pili, mnamo 05/06/2014 Polisi Wilaya ya Buguruni mkoa wa kipolisi Ilala kwa kushirikiana na bwana BAKARI  YUSUF, Miaka 33, Mhifadhi Wanyamapori Makao Makuu, Mkazi wa Mbezi Beach, walifanikiwa kukamata vipande 28 vya meno ya Tembo vyenye thamani ya fedha za kitanzania  milion mia mbili sabin na tano  laki tano na elfu hamsini nyumbani kwa DOMINICK  KORINELI maarufu  KOMBE, Miaka 35, Mkazi wa Tabata Kisukuru. 

Walipofanya  upekuzi katika nyumba hiyo ,ambapo kwenye chumba kimoja cha uwani  cha bwana HERBERT   REVIL MACHAKA, Miaka 30, mkazi wa Morogoro, ndipo  kilipitikana kipande 1 cha jino la Tembo.

 Upekuzi uliendelea kwenye Stoo na Jiko  na walipata vipande 27 vya meno ya tembo na kufanya jumla ya vipande hivyo kuwa 28 kwa tukio la pili hivyo kufanya idadi ya vipande kufikia 54 Watuhumiwa wanaendelea kuhojiwa ili kubaini mtandao mzima wa ujangili huu unaomaliza rasilimali za taifa.  na mara baada ya upelelezi kukamilika watafikishwa  mahakamani

No comments:

Post a Comment