Thursday, June 12, 2014

WATU WAWILI WANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI DAR ES SALAAM MARA BAADA YA KUPATIKANA NA SARE ZA JESHI LA WANANCHI TANZANIA (JWTZ )KINYUME CHA SHERIA.


Mnamo Tarehe 01.06.2014 huko maeneo ya Mbagala Maji Matitu,Kata ya Chamazi , Wilaya ya  Mbagala, Mkoa wa Temeke, polisi walipokea taarifa toka kwa mtoa taarifa mwenye namba  P.8464 cheo cha  Meja FAUDHI   OMARI ALLY wa Kikosi cha Anga Makao Makuu cha JWTZ,

akitaarifu  kwamba amemkamata mtu mmoja aitwaye FRANCIS   MARTINE KILALA, Miaka 24, Mkazi wa Kawe akiwa amevaa sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania zenye  cheo cha LUTENI akiwa ndani ya Daladala. 

  mtu huyo alipohojiwa alikiri kuwa yeye sio askari na alipopekuliwa alipatikana na vitambulisho 3 ambavyo  kimoja chenye  no. PT.86876 PTE THOMAS MWITA kikiwa kimewekwa picha yake ya mtuhumiwa , na viwili vikiwa vya watoto wa askari vyenye namba  Z0186 MTUYO OMARI MAGULU na Z0116  MAULIDI ISSA HASSAN ambacho ni cha mtoto wa askari mwenye namba P.8487 NF MANDAGO. Mtuhumiwa anashikiliwa kwa mahojiano. Upelelezi juu ya wapi amepata sare hizi unaendelea.

Aidha amekamatwa mtu mwingine aitwaye DAUDI  MADA maarufu kama  PAKIMERO, Miaka 30,  Mkazi wa Tandika Nyambwera akiwa na sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) zikiwemo
·       FULANA NA SHATI YA KIJANI
·       SURUALI NA SHATI ZA MABAKA
·       JOZI MOJA YA BUTI ZA JESHI
·       KOFIA MBILI ZA RANGI YA KIJANI
·       BEGI MOJA LA NGUO (MABAKA)

TAARIFA ZA USALAMA BARABARANI KANDA MAALUM KUANZIA TAREHE 1/6/2014 – 12/6/2014.
·       Idadi ya makosa yaliyokamatwa ilikuwa 7176
·       Pikipiki zilizokamatwa                            462
·       Daladala zilizokamatwa                           4136
·       Magari mengine                              2441
·       Hela za tozo                                              215,280,000/=  

No comments:

Post a Comment