Monday, July 28, 2014

Kuweni Wabunifu Zaidi - Prof. Mchome

Displaying DSC07933.JPG
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome akiongea na Watumishi wa wizara yake katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (Julius Nyerere International Convention Centre), Ijumaa 18 Julai, 2014 ikiwa ni utaratibu aliojiwekea wa kukutana na watumishi hao na kujadiliana namna bora zaidi ya kuboresha utendaji kazi katika wizara.
 Displaying DSC08012.JPG
Mmoja wa Watumishi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Grace Naburi akizungumza katika kikao cha Wafanyakazi wa wizara hiyo na Katibu Mkuu wao Profesa Sifuni Mchome.
Displaying DSC07924.JPG
Watumishi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wakiimba wimbo wa Mshikamano katika kikao cha Wafanyakazi wa wizara hiyo na Katibu Mkuu wao Prof. Sifuni Mchome.
 
Displaying DSC08015.JPGMmoja wa Watumishi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi akizungumza katika kikao cha Wafanyakazi wa wizara hiyo na Katibu Mkuu wao Profesa Sifuni Mchome.
 


Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome

amewataka Watumishi wa Wizara hiyo kuwa wabunifu zaidi na kuhakikisha

kuwa wanachokibuni kiwe kinatekelezwa na kuchukua hatua kwa wasiotekeleza

maelekezo ya kisera pamoja na kuwazawadia wanaotekeleza kwa ufanisi

maelekezo yanayotolewa.

“Watumishi wa Wizara hii tunatakiwa tujiulize tunafanya ubunifu gani ili kuhakisha

wahitimu katika ngazi mbalimbali wanapata maarifa yanayotakiwa na wanaoweza

kusaidia nchi katika kuleta maendeleo katika nyanja mbalimbali,” alisema Profesa

Profesa Mchome alikuwa akizungumza na Watumishi wa Makao Makuu na Taasisi

zilizoko chini ya Wizara hiyo katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius

Nyerere (Julius Nyerere International Convention Centre), Ijumaa 18 Julai, 2014

ikiwa ni utaratibu aliojiwekea wa kukutana na watumishi hao na kujadiliana namna

bora zaidi ya kuboresha utendaji kazi katika wizara.

Aidha, Profesa Mchome alizungumzia umuhimu wa kuboresha Muundo wa Wizara

hiyo ili kuwezesha namna bora ya kutekeleza majukumu yake baada ya ugatuaji wa

uendeshaji na usimamizi wa shule za Sekondari kwenda kwenye Halmashauri chini

ya Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI na kwa kufuata Hati Idhini iliyounda Wizara ya

Elimu na Mafunzo ya Ufundi iliyotolewa na Mheshimiwa Rais, Desemba 2010.
 

No comments:

Post a Comment