Monday, February 6, 2017

Buhari ataka kupata matibabu zaidi Uingereza

Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari amelitaka bunge la nchi hiyo kumuongezea likizo yake, ya kupata matibabu.
Ametoa taarifa hiyo akiwa nchini Uingereza kwa ajili ya vipimo vya afya yake.
Rais Buhari aliondoka nchini Nigeria wiki mbili zilizopita na alitarajiwa kurudi mjini Abuja jana.
Taarifa iliyotolewa na ofisi yake imesema, ameshauriwa na madaktari kumaliza matibabu na kusubiri matokeo ya vipimo alivyopima.

No comments:

Post a Comment