Thursday, June 4, 2015

MH LOWASA ACHANGIAWA FEDHA ZA KUCHUKUA FOMU NA WANA CCM MKOA WA TABORA


Mzee wa CCM wilaya ya Urambo mkoani Tabora, Yusuf Bundala Kasubi, (kulia),  akimkabidhi Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa,  zaidi ya shilingi milioni  moja, zilizochangwa na wanachama wa CCM mkoani Tabora, ili kumuwezesha mtangaza nia ya kuwania urais kupitia CCM, Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, ili azitumia kulipia ada ya kuchukua fomu za kuwani urais kupitia chama hicho. Hafla ya kukabidhi fedha hizo ilifanyika nyumbani kwa Mtangaza nia huyo, mjini Dodoma JAlhamisi Juni 4, 2015. Badaaye jioni Lowassa anatarajiwa kuchukua fomu hizo, makao makuu ya CCM mjini Dodoma.
Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, ambaye tayari ametangaza nia ya kuwania urais kupitia CCM, Edward Lowassa, akisalimiana na ujumbe wa wana CCM kutoka mkoani Tabora, walipofika nyumbani kwake mjini Dodoma leo Alhamisi Juni 4, 2015, ili kumpatia mchango wao wa nkumuwezesha kulipia ada ya fomu ya kuwani urais.
Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, ambaye tayari ametangaza nia ya kuwania urais kupitia CCM, Edward Lowassa, akisalimiana na ujumbe wa wana CCM kutoka mkoani Tabora, walipofika nyumbani kwake mjini Dodoma leo Alhamisi Juni 4, 2015, ili kumpatia mchango wao wa nkumuwezesha kulipia ada ya fomu ya kuwani urais.
Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, ambaye tayari ametangaza nia ya kuwania urais kupitia CCM, Edward Lowassa, akiwashukuru wana CCM kutoka mkoani Tabora, baada ya kumkabidhi mchangio wa zaidi ya shilingi milioni 1 ili azitumia kulipia ada ya kuchukua fomu za kuwania urais katika hafla iliyofanyika nyumbani kwake mjini Dodoma, leo Alhamisi Juni 4, 2015.
Katibu wa Uchumi na Fedha wa CCM wilaya ya Nzega mkoani Tabora, Majaliwa Bilali, (kulia), akizungumza sababu zilizowapelekea wana CCM mkoani humo kuchanga fedha za kumuwezesha Mtangaza nia ya kuwania urais kupitia CCM, Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, (kushoto), wakati wa hafla fupi ya kukabidhi mchango huo wa shilin gi milioni 1 zilizofanyika nyumbani kwa mtangaza nia huyo, mjini Dodoma, Alhamisi Juni 4, 2015. Badaaye jioni Lowassa anatarajiwa kuchukua fomu hizo, makao makuu ya CCM mjini Dodoma.

No comments:

Post a Comment