MKURUGENZI wa
jiji la Mwanza,Willson Kabwe juzi alipanda kizimbani katika mahakama ya mwanzo
Maromboso jijini Arusha,kutoa utetezi juu ya madai ya kutaka kupora mali za marehemu
mdogo wake,John Mkenga aliyefariki hivi karibuni kwa ajali ya gari na kuacha
mke na watoto wanane.
Kesi hiyo ya
mirathi namba 42 ya 2012 inasikilizwa na hakimu Mwanaidi Lemmy wa mahakama
ya mwanzo,ambapo Kabwe anapinga mke wa marehemu,Blandina Mkenga kuwa msimamizi
wa mali za marehemu mumewe na kudai kuwa hana sifa za kisheria .
Akitoa utetezi
huo mbele ya hakimu Lemmy,Kabwe alidai kuwa kikao cha ukoo kilichofanyika
februari 14 mwaka huu kilimpitisha kama msimamizi mkuu wa mali za marehemu.
Upande wa mjibu
maombi ambaye ni mke wa marehemu, Blandina Mkenga anadai kuwa hoja ya Kabwe haina
msingi kwani kikao kilichofanyika kumteua
Kabwe kuwa msimamizi wa mirathi ni cha
kimila na kililenga kumkandamiza mwanamke kusimamia mali za marehemu mumewe.
''kama wewe
unauchungu na familia ya marehemu mdogo wako umewahi kufika mara ngapi hapa
nyumbani kuijulia hali familia na unajua tunaishije,ivi unahabari kwamba hadi
sasa watoto hawaendi shule kwa kukosa ada''alisema na kuongeza.
''kwanini
unathamini zaidi mali za marehemu kuliko familia na watoto wameachwa bila
msaada huku wewe ukidai umeteuliwa kusimamia mali za marehemu''alisema Blandina
baada ya hakimu Lermmy kumpa idhini ya
kumuuliza swali Kabwe ambaye ni
shemeji yake
Alizidi kuieleza
mahakama kwamba ,Kabwe na wenzeke akiwemo kaka yao mkubwa,Jacob Mkenga
wanalengo la kupora mali za marehemu kwa kutumia mgongo wa kimila ,hivyo
aliiomba mahakama itengue maamuzi hayo na kumpitisha yeye kuwa ndiye msimamizi
halali wa mali za Mumewe.
Shahidi wa
upande wa mjibu maombi,Elitabu Mkenga ambaye ni mdogo wa marehemu alimtaka kaka
yake, Kabwe kuacha ubinafsi na kudai kwamba analengo la kutaka kupora mali za
mdogo wake kwani alishazoea kufanya ufisadi kwenye halmashauri.
‘’ivi wewe
hujatosheka na ufisadi unaoufanya huko Mwanza unataka pia kufanya ufisadi
kwenye mali za marehemu mbona mimi ni mdogo wa marehemu sipiganii mali hiyo
kwani mimi sihitaji mali, najua ni mali za watoto sasa wewe unachotaka nini’’alimuuliza
swali Kabwe
Hatua hiyo
ilichafua hali ya hewa mahakamani hapo ambapo wanandugu hao walianza
kushambuliana kwa maneno makali huku kabwe akimweleza mdogo wake kwamba
anampango wa kumridhi mke wa marehemu kwani amehama nyumbani kwake na kuhamia
kwenye familia ya marehemu.
Malumbano hayo yalizimwa
na hakimu Lemmy baada ya kuwataka wasizungumzia masuala ya nyumbani kwao mahakamani hapo kwani hayana msaada wowote
katika kesi hiyo.
‘’unajua mimi
nawashangaa sana mnapoleta malumbano ya masuala ya nyumbani kwenu hapa mahakamani , hayo mambo ya familia yenu
hatuyahitaji katika kesi hii,tafadhili nendeni kwenye kesi ya msingi
iliyotuileta hapa’’alisisitiza hakimu Lemmy.
Akisisitiza
mahakamani hapo Kabwe aliieleza mahakama kwamba anataka imwidhinishe kuwa
msimamizi halali wa mali za marehemu ili aweze kudhibiti mali hizo zisiporwe kwani tayari anaoushahidi wa wazi
kwamba siku chache baada ya marehemu kufariki ndugu wa upande wa mke wa marehemu
walimiminika kwenye mgodi wa marehemu na kupora madini ya Tanzanite yenye thamani
kubwa.
‘’mheshimiwa
hakimu ninao ushahidi wa wazi kabisa kwamba siku chache tu baada ya marehemu
kufariki ndugu wa upande wa mke wa marehemu walivamia mgodi wa madini uliopo
Mererani na kupora kiasi kikubwa cha madini’’alisema Kabwe
Hata hivyo
hakimu Lemmy alimtaka Kabwe kuleta hoja hiyo baada ya kumalizika kwa kesi ya
msingi iliyofunguliwa kwani hoja hiyo haihusiani katika kesi hiyo ya msingi
inayoendelea hapo mahakamani.
Hakimu Lemmy
alimtaka Kabwe kuzitaja mali zilizoachwa na marehemu mdogo wake kwa ujumla ,ambapo Kabwe alizitaja kuwa ni pamoja na
mgodi wa madini ya Tanzanite,Kiwanda cha kutengeneza nafaka ya binadamu na
mifugo.
Mali zingine ni
Godauni makubwa 7 yaliyopo Kisongo jijini Arusha,migodi ya madini ya dhahabu iliyopo
mkoani Tanga,Nyumba za kuishi zilizopo maeneo tofauti nje ,viwanja vya
kuendeleza ,magari ,Fedha zilizopo Benki tofauti na mali zingine alizodai
hazifahamu.
Mara baada ya
utetezi wa pande zote wakiwemo mashahidi ,hakimu Lemmy aliahirisha kesi hiyo
hadi Juni 22 mwaka huu, itakapotole hukumu na kuzitaka pande zote kuhakikisha
zinafika mahakamani hapo.
Awali Kabwe akishirikiana na ndugu wengine walileta
pingamizi mahakamani la kutaka mahakama isitishe taratibu za mirathi kwa madai kuwa mke wa marehemu hana mamlaka ya
kusimamia mirathi.
Baada ya hatua
hiyo,Kabwe alipeleka barua ya pingamizi kwa hakimu wa mahakama hiyo,Mwanaidi
Lemmy ya tarehe 12/4/2012 ya kutaka shauri la mirathi namba 42/2012
lililofunguliwa na mke wa marehemu,kusitishwa mchakato wote wa kuendelea
kusikiliza shauri hilo.
Katika barua
hiyo Kabwe alitoa sababu sita na moja ya sababu ni kuitaka mahakama hiyo
isitishe kuwasikiliza kwani yeye hakuwa na taarifa rasmi kwani yeye ndiye
mwenye mamlaka aliyeteuliwa kusimamia mirathi ya mdogo wake,kama ilivyoamuliwa
na kikao cha ukoo kilichoketi Februal 14 mwaka huu na kwamba mke wa merehem,u
hajawahi kuteuliwa kusimamia mirathi na ukoo.
No comments:
Post a Comment