Monday, June 11, 2012

Kagere: Naipenda Yanga kuliko Simba

MSHAMBULIAJI wa timu ya Taifa ya Rwanda(Amavubi), Meddie Kagere amekiri kufanya mazungumza na klabu ya Yanga ya jijini Dar es Salaam na amefanya hivyo kutokana na kuvutiwa na klabu hiyo ya Jangwani.Hata hivyo, hatma ya mazungumzo hayo anatarajia kuyaanika hadharani baada ya pambano la kusaka tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia mwaka 2012 kati ya Rwanda na Benin mwishoni mwa wiki hii.


Akizungumza na Mwananchi kwa simu toka Kigali, Rwanda, Kagere anayeichezea Polisi Rwanda, alisema amepokea ofa kadhaa toka klabu za ndani na nje, lakini mpango wake wa sasa ni kujiunga na Yanga.
"Niweke wazi kwamba, Yanga wananihitaji na tayari nimefanya nao mazungumzo ya awali. Upo uwezekano nikajiunga nao ingawa hatujaafikiana moja kwa moja kwani nimewaambia wasubiri.

"Siyo Yanga tu, zipo klabu nyingi zinanihitaji ikiwemo Simba ya hapo Tanzania lakini zaidi ningependelea kucheza Yanga kuliko Simba," alisema Kagere na kuongeza kuwa:

"Huwa nazungumza na Haruna (Niyonzima) kuhusu ligi ya Tanzania ndiye yeye ndiyo anayenishawishi kuja. Mimi na yeye tunaelewana tunapocheza pamoja timu ya taifa na bila shaka ushirikiano wetu na wachezaji wengine tunaweza kuipa Yanga mafanikio."





No comments:

Post a Comment