Watu kadhaa wanahofiwa kufariki dunia katika maporomoko ya arthi Mashariki mwa Uganda. Hii ni kwa mujibu wa maafisa eneo hilo.
Katibu wa Shirika la Msalaba Mwekundu Uganda Michael Richard Nataka ameambia BBC kwamba katika kijiji komoja nyumba 15 zimefunikwa huku watu wengi wakikwama kwenye makaazi yao huko Bududa.
Tayari watu 20 wamethibitishwa kufa na idadi hii huenda ikaongezeka.
Awali maafisa walisema watu kati ya 20 hadi 100 waliangamia. Eneo hilo limeshuhudia mvua kubwa katika siku za karibuni.
Hapo Agosti mwaka jana watu 24 walikufa baada ya mvua kubwa kusababisha maporomoko ya arthi katika Wilaya ya Bulambuli Mashariki mwa Uganda. Mwaka 2010 watu 100 walikufa katika Wilaya Bududa baada ya maporomoko ya ardhi.
No comments:
Post a Comment