Baraza la mawaziri nchini Kuwait limejiuzulu.
Kujiuzulu huko leo kumekuja siku kadhaa baada ya
mahakama kuu kubatilisha uchaguzi wa bunge.
Kituo kimoja cha binafsi cha televisheni Al-Rai, Kimesema kwamba baraza hilo la mawaziri liliwasilisha hati ya kujiuzulu kwa Mfalme wa nchi hiyo, lakini hapakutolewa taarifa zaidi.
Baraza hilo liliundwa miezi minne tu baada ya uchaguzi wa bunge mwezi Februari mwaka huu, ambapo upinzani ulipata ushindi mkubwa na wingi wa viti bungeni.
Lilikuwa ni baraza la mawaziri la tisa katika Falme hiyo yenye utajiri wa mafuta tokea Februari 2006
. Mawaziri wawili katika baraza hilo lililokuwa na mawaziri 16, walilazimika kujiuzulu wiki chache zilizopita, baada ya kushinikizwa na wabunge.
Kituo kimoja cha binafsi cha televisheni Al-Rai, Kimesema kwamba baraza hilo la mawaziri liliwasilisha hati ya kujiuzulu kwa Mfalme wa nchi hiyo, lakini hapakutolewa taarifa zaidi.
Baraza hilo liliundwa miezi minne tu baada ya uchaguzi wa bunge mwezi Februari mwaka huu, ambapo upinzani ulipata ushindi mkubwa na wingi wa viti bungeni.
Lilikuwa ni baraza la mawaziri la tisa katika Falme hiyo yenye utajiri wa mafuta tokea Februari 2006
. Mawaziri wawili katika baraza hilo lililokuwa na mawaziri 16, walilazimika kujiuzulu wiki chache zilizopita, baada ya kushinikizwa na wabunge.
No comments:
Post a Comment