Katika ripoti mpya ya shirika la
kutetea haki za binadamu la Amnesty International, serikali ya Syria
imeshutumiwa kwa uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu.
Katika mji wa Aleppo, watafiti wa Amnesty waliona vikosi vya serikali ya Syria na wanamgambo washirika wake kwa kuyafyatulia risasi maandamano ya amani, na kuwaua na kuwajeruhi waandamanaji na wapita njia.
Afisa mwandamizi mshauri wa migogoro katika shirika la Amnesty, Donatella Rovera, amesema serikali ya Syria imekuwa ikiwalenga hususan raia na kwa makusudi:
No comments:
Post a Comment