Hata hivyo, maandamano hayo yamepingwa na Baraza kuu la Uongozi la Libya, ambalo katika taarifa yake limekiita kitendo hicho ni kiovu na kisichotarajiwa kutokea kwa ubalozi wa Marekani mjini Benghazi.
Tukio la maandamano nchini Libya linafuatia tukio kama hilo lililofanywa na waandamanaji mjini Cairo hapo jana ambapo waandamanaji wapatao 3,000, wengi wao wakiwa ni wa kundi la Salafi, walipoandamana kwenye ubalozi wa Marekani nchini humo kupinga filamu kama hiyo inayomkashifu Mtume Muhammad (S.A.W)
Mamia ya watu waliuzingira ubalozi wa Marekani na kisha mmoja wao kuiteremsha bendera ya marekani na kupandisha bendera yanye rangi nyeusi iliyo na alama ya kiislamu, na kisha kusema Mungu ni mmoja na Muhammad ni Mtume wa Mungu.
No comments:
Post a Comment