Thursday, September 13, 2012

Filamu ya kashfa kwa Mtume




Rais wa Libya, Mohammed el-Magarief (katikati). Rais wa Libya, Mohammed el-Magarief (katikati).
Filamu hiyo ambayo ndicho kitovu cha machafuko na maandamano hayo imeandaliwa na raia wa Marekani mwenye asili ya Israel ambaye anaueleza Uislamu kama kidonda ndugu na kumuonesha Mtume Muhammad (S.A.W) akilala na wanawake, kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa na gazeti la Wall Street Journal la Marekani.

Awali, mjni Tripoli, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Libya, Wanish al Sharif, aliliambia shirika la habari la Ufaransa (AFP), kuwa ofisa mmoja wa Marekani aliuawa na mwengine kujeruhiwa wakiwa mikononi mwa waandamanaji huku wafanyakazi wengine wakiokolewa na wapo salama. Sharif alisema waandamanaji waliuvamia ubalozi huo wa Marekani na kuanza kurusha risasi hewani kabla ya kuingia ndani na kuanza kuwashambulia wafanyakazi.


Msemaji wa wizara hiyo, Abdelmonoem al-Horr, alisema guruneti lililorushwa kwenye ubalozi huo liliripuka kwenye bustani iliyoko karibu na ubalozi huo. Watu walioshuhudia tukio hilo wamesema wavamizi waliiteremsha bendera ya Marekani iliyokuwepo kwenye ubalozi huo na kisha kuanza kuuchoma moto ubalozi huo.

No comments:

Post a Comment