Awali, mjni Tripoli, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Libya, Wanish al Sharif, aliliambia shirika la habari la Ufaransa (AFP), kuwa ofisa mmoja wa Marekani aliuawa na mwengine kujeruhiwa wakiwa mikononi mwa waandamanaji huku wafanyakazi wengine wakiokolewa na wapo salama. Sharif alisema waandamanaji waliuvamia ubalozi huo wa Marekani na kuanza kurusha risasi hewani kabla ya kuingia ndani na kuanza kuwashambulia wafanyakazi.
Msemaji wa wizara hiyo, Abdelmonoem al-Horr, alisema guruneti lililorushwa kwenye ubalozi huo liliripuka kwenye bustani iliyoko karibu na ubalozi huo. Watu walioshuhudia tukio hilo wamesema wavamizi waliiteremsha bendera ya Marekani iliyokuwepo kwenye ubalozi huo na kisha kuanza kuuchoma moto ubalozi huo.
No comments:
Post a Comment