"Nimefadhaishwa na mashambulizi dhidi ya ubalozi wetu nchini Libya na Misri na mauaji ya balozi wetu. Ni aibu kwa utawala wa Obama kutoa jawabu iliyotoa kwa kutokulaani mashambulizi kwenye balozi zetu bali kusimama upande wa waandamanaji." Alisema Romney.
Hata hivyo, mapema wizara ya mambo ya nje ilitoa tamko la kulaani vikali mashambulizi hayo. Waziri wa Mambo ya Nje, Hillary Clinton, alisema amezungumza na Rais Mohammed al-Magariaf wa Libya juu ya mashambulizi hayo na kwa pamoja wakakubaliana kuchukua hatua za haraka.
No comments:
Post a Comment