Wednesday, September 19, 2012

NATO kupunguza operesheni Afghanistan

Jumuiya ya kujihami ya NATO inapunguza operesheni za pamoja nchini Afghanistan kufuatia mfululizo wa mashambulizi ya ndani na ghadhabu iliyosababishwa na filamu inayoudhalilisha Uislamu.

Katibu mkuu wa jumuiya hiyo, Anders Fogh Rasmussen, amesema hatua hiyo inalenga kupunguza vifo zaidi vya wanajeshi wa mataifa ya magharibi wanaouwawa na Waafghanistan.


 Hata hivyo Rasmussen amesema ushirikiano utaendelea katika ngazi zote na kwamba jumuiya ya NATO bado imejitolea kwa dhati kuona Waafghanistan wanasimamia usalama wao kufikia mwisho wa mwaka 2014.

No comments:

Post a Comment