Saturday, March 30, 2013

RAIS KIKWETE, ATEMBELEA ENEO LILIPOTOKEA AJALI YA KUANGUKA GHOROFA JIJINI DAR



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa  mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es salaam jana akiwa ameongozana na mkewe Mama Salma Kikwete kujionea mwenyewe jengo lililoporomoka asubuhi saa mbili na nusu jana Machi 29, 2013 ambapo hadi Rais anafika mahali hapo saa saba kamili watu wawili walikuwa wamethibitishwa kuwa wamekufa na wengine 19 kujeruhiwa, wawili wakiwa mahututi. Juhudi zilikuwa bado zinaendelea  kuokoa watu wanaosadikiwa kunaswa kwenye kifusi cha jengo hilo lililokuwa limefikia ghorofa ya 15, likijengwa ubavuni mwa Msikiti wa Shia Ithnaasheri.







 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo toka kwa Mkuu wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam Bw. Suleiman Kova na Mkuu wa Mkoa huo Mhe saidi Meck Sadiki katika eneo la  jengo lililoporomoka mtaa wa Indira Ghandi jijini Dar es salaam   




Hadi kufikia leo asubuhi  ni maiti nne tu  ndizo zimedhibitishwa kuokolewa na jeshi la polisi na bado jeshi la wananch tanzania ,polisi na vikosi mbali mbali pamoja na mashirika mbali mbali pamoja na ya watu binafsi bado walikuwa wakiendelea kutoa  misaada ya hali na mali ili kuhakikisha kuwa zoezi la uokoaji lina kamilika kwa muda muafaka.

wakati zoezi hilo likiwa linaendelea tayari jeshi la polisi limedhibitisha kumkata mmliki wa jengo hilo mara baada ya kujisalimisha m wenye mikononi mwa  polisi pia jeshi la polisi limedhibitisha kuwatia mikoni  maafisa watatu walikuwa wakifuatilia ujenzi wa jengo hilo


maafisa hao  wanaoshikiliwa ni pamoja na mhandisi mkuu wa jengo hilo ,mhandisi wa manispaa pamoja na mkaguzi wa jengo hilo ili waweze kusaidi uchunguzi zaidi kuhusu kuanguka kwa jengo hilo lenye urefu wa ghorofa 15

No comments:

Post a Comment