Saturday, May 25, 2013

JESHI LA POLISI KANDA MAALUM DAR ES SALAAM LIMEWAKAMATA MAJAMBAZI WATANO ,SMG MOJA ,BASTOLA 2 NA PINGU.

Jeshi la  polisi kanda maalum limefanikiwa kukamata majambazi watano ,Smg moja,Bastola  mbili,magari mawili ,matairi kumi,pikipiki moja  pamoja na pingu.

Akiongea na waandishi wahabari ofisini kwake kamanda wa kanda maalum DCP Suleiman Kova amesema jeshi la polisi kanda maalum  mnamo tarehe 22/05/2013 majira ya saa tano asubuhi  limefanikiwa kukamata majambazi 5 waliopora maeneo ya  Mbagala rangi tatu ,wilaya ya Temeke  muda mfupi  baada ya kupora  .

Tukio hilo lilitolewa taarifa na  mfanyabiashara    amabye aliibiwa  alipokuwa dukani mwake katika duka la kuuza bia na ghafla  alivamiwa na majambazi watano  watatu kati yao  akiwa na silaha kubwa na bastola mbili na kuporwa pesa taslim  milioni arobain na sita  (46,000,000.) pesa ambazo alikuwa ameweka kwenye box tayari kuzipeleka kwenye benki ya Boa.


Majambazi hao walikuja kwa kutumia piki piki  mbili aina ya boxer zenye namba za usajili T.311 CGE rangi nyekundu   na walimtishia mfanyabiashara huyo  bila kufyetua risasi na kufanikiwa kuiba kiasi hicho cha pesa na baada ya polisi kupata taarifa hizo waliwakamata  maeneo ya Chamazi na majini yao :

1;Benard Yohana Mashamba
2;Steven Thadeo
3;Adam Isidory
4;John Masambo Benja
watuhumiwa wote mara baada kuhojiwa na jeshi la polisi walimtaja mwenzao John Tesha aliyekimbia na pesa hizo

katika tukio lingine jeshi la polisi kanda maalum Dar es salaam limefanikiwa kukamata bunduki aina ya Smg  no wa2608199 na magazine moja  isyo na risasa huko maeneo ya Mbagala kimbangulile   na polisi inawashikilia  Saidi Ally na maneno Yahaya Mohamed  wakituhumiwa  kwa matukio ya unyang’anyi  kwa  kutumia silaha hiyo wakitumi ausafiri wa gari lenye namba za usajili  T 323 CFN na  T 289 BYL .

polisi inamshikilia  Erick Innocent Mbise  kwa tuhuma za kukutwa na  piki piki  m oja  aina ya Fekon  rangi nyeusi  noT 155 CHX  pamoja na pingu  na mt uhumiwa  ametambuliwa na matukio mbali mbali ya wizi wa piki piki.
Photo
HIZI PIKI PIKI ZILIZOKAMTWA KWA MAKOSA MBALI MBALI

wakati huo huo mnano tarehe 18/05/2013 katika msako  ilipatikana  gari  aina ya toyota corala  ambapo  namba yake halali ni  T 509 BZQ ambayo  iliibiwa tarehe  16/02/2013 nyumbani kwa  Salome Edward  Kange  kwa kutumia  funguo bandia na  polisi inawashikilia Ally  Musa  na Rebeka  Mpumba  kwa tukio hilo.
Photo
 PICHA JUU NI GARI LILOKAMATWA BAADA YA KUIBIWA NA HIZO NAMBA HAPO NI NAMBA ZA PIKI PIKI
katika tukio la pili gari namba T 861 BGU  toyota noah yenye namba za usajili T 897 BLV  liloibiwa tarehe 26/01/2013 nyumbani kwa  Honory Kilipo Kobero  huko Kimara Temboni  lilikamatwa  tarehe 10/05/2013 huko Magomeni  na polisi inawashilikilia   watuhumiwa wawili  ambao ni Augustino Kirunde Sanga na  Jeremiah Nzashe Eliasi kwa kuhusika na tukio hilo.
Photo
Aidha jeshi la polisi kanda maalum inawashikilia  Elias Mohamed ,Nasiri Abdi na Deo  John kwa tuhuma za kukutwa wakipakia matairi kumi kwenye  gari no T 346 BVB matairi ambayo yaliibiwa katika godown.

kamanda Suleimani Kova amemamliza kwa kusema jeshi la polisi limejizatiti kutoa  ulinzi na usalama kwa raia wote  na kukanusha habari zilizozagaa kuwa walishindwa kutoa ushirikiano katika tukio la wizi wa milioni arubain na  sita kwa kuonyesha silaha zilizokamatwa katika tukio hilo na kusema  polisi linawashikilia watumiwa wa tukio hilo huku wakifanya msako mkali kumkamata jambazi aliekimbia na fedha hizo.



No comments:

Post a Comment