Friday, May 31, 2013

TIGO NA FASTJET YAZINDUA HUDUMA YA NUNUA TIKETI YA FASTJET KWA KUPITIA HUDUMA YA TIGO YA NUNUA NA UZA CHOCHOTE NA TIGO PESA

MENEJA MASOKO WA TIGO NA MENEJA WA FASTJET BWANA Tim Lee-Foster.
MENEJA MASOKO WA TIGO NA MENEJA WA FASTJET BWANA TIM LEE-FOSTER 



PICHA YA PAMOJA TIGO NA FASTJET


WAANDISHI WA HABARI MBALI MABLI WAKIFUATILIA MAELEZO YA MENEJA MASOKO WA TIGO BWANA WILLIM MPINGA
Kampuni ya simu za mikononi Tigo Dar esalaam imezindua huduma mpya ya kununua tiket kutoka shirika la ndege na Fast jet  ikiwa na moja kati ya huduma zake za nunua na uza chochote ukiwa na  TIGO PESA.

Akiongea na waandishi wa habari jana katika hotel ya  Atlantis  ya jijin Dar es alaam Meneja mauzo wa Tigo bwana William Mpinga amesema  wamezindua rasmi huduma ya kununua tiket za kusafiria za ndege za shirika la fastjet  mara baada ya shirika hilo kuona mafaniko  ya huduma ya tigo  pesa na huduma ya Nunua na uza chochote na Tigo pesa kuzinduliwa hivi majuzi.

Muungano huo wa kirafiki wa biashara baina ya Tigo na Fastet unalengo la kumrahisishia Mtanzania  katika kupata huduma za fast jet na kuokoa muda wa kwenda  ofisini kuandaa tiket ya safari , a kusema huduma hiyo sasa inapatikna mikononi mwako kwa kutumia simu yako yenye lain ya tigo ambayo imeunganishwa na huduma ya Tigo Pesa.

Ili kupata huduma ya  kununa tiket ya Fastjet ni rahisi sana kwako mtumiaji wa Tigo piga *150*01 na ufuate maelekezo ambayo yatakupeleka mpaka  uweze kununua tiket  yako ya fast jet popote pale ulipo nchini Tanzania

Nae akionge baada ya uzinduzi huo wa nunua tiket ya fast jet na tigo pesa meneja wa fast jet bwana TIM LEE-FOSTER  amesema  bado wataendelea kuleta huduma mpya zaidi na nzuri  kutoka Fastjet na kusema ,pamoja na mafaniko makubwa waliopata baada ya kuwa na huduma ya nunua tiket na fastjetbado wanamalengo makubwa ya kupanua biashara ya Fastjet kwa kuwa karibu na jamii nzima ndio sababu wakakubali kuungana na Tigo kwani tigo  ipo mstari wa mbele  kutoa huduma kwa jamii ya Tanzania wakati wote.

Akimalizia kuzindua muungan huo wa kibiashara baina ya fastjet na Tigo Tanzania, Mpinga amesema hii ni hatua kubwa kufikiwa baina Tigo na Fastjet na kuwaahidi watumiaji wa Huduma za tigo huduma bora kwa wateja wake waote waliojiunga na huduma ya TIGO PESA.

UNANGOJA NINI JIUNGE NA TIGO PESA UPATE HUDUMA BORA KUTOKA  TIGO PESA

No comments:

Post a Comment