Monday, June 17, 2013

GUDLUCK LARONYA WA CCM AWA MSHINDI KITI CHA UDIWANI MAKUYUNI ASHINDA KWA ZAIDI YA 90%

Chama cha Mapinduzi kimeibuka Kidedea jioni jana baada ya Gudluck Laronya aliyekuwa Mgombea wa Udiwani Kata ya Makuyuni Monduli Arusha Kumbwaga mwenzake wa CHADEMA kwa zaidi ya Asilimia 90 ya kura zote zilizohesabika jana.
Akiyatangaza Matokeo hayo Majira ya Saa Moja na dk. 20 Usiku huu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Bw. Twalib Mbasha amemtangaza rasmi Bw. Gudluck kuwa ndiye Diwani Mpya wa Kata ya Makuyuni kwa kupata 1543 dhidi ya Mgombea wa CHADEMA  Japheti Lairumbe aliyepata kura 360 TU.

Idadi ya Waliojiandikisha ni 5027
Idadi ya Waliopiga Kura 1920
Idadi ya Kura Halali ni 1903
Idadi ya kura Zilizoharibika ni 17

No comments:

Post a Comment