Tuesday, July 9, 2013

DR VICTORIA KISYOMBE AWATAKA WANAWAKE KUPIGA VITA RUSHWA NA BENKI KUWEKEZA VIJIJINI

Taasisi mbali mbali za kusaidia wanawake nchini Tanzania wametakiwa kujitangaza kwa jamii na kwa kwa wananwake wenyewe ili wanawake waweze kuzifaham na kutumia fursa zinazotolewa na taasisi hizo katika kuinua maendeleo kwa kupitia kundi la wanawake  wanaojiunga katika jamii ili kujikomboa kiuchumi. 

Hayo yamesemwa na askofu mkuu wa kkkt dayosis ya  Mashariki na pwani na makamu wa rais wa muungano wa makanisa ya kiluther duniani  Dr Alex Malasusa alipohudhuria mkutano wa majadiliano wa  kusaidia wanawake kwa kuwawezesha mambo ya kifedha ili kuweza kuinua uchimi nchini Tanzania .

Amezidi kuwaomba wanawake kutumia taasis za kusaidia wanawake  na hasa amewaomba wanawake kuwa waaminifu katika kurudisha mikopo waliyopewa ili kuwezesha taasisi hizo kuweza kuwasaidia wanawake wengi kuweza kujikwamua na umasikini na kuleta maendeleo nchini.

Kwa upande wake mwanzilishi wa taasisi ya  kutoa mikopo na kuwa saidia wananwake katika nyanja mbali mbali za kimaendeleo iitwayo SELFINA  ,DR VICTORIA KISYOMBE amesema kama Watanzania wanataka kupata maendeleo ni lazima wapige vita Rushwa ili  kuweza kufikia malengo ya maendeleo.


Akifafanua jinsi rushwa inavyorudisha maendeleo Dr kysombe na mwanzilishi wa taasis ya Selfina ,amesema rushwa ni adui mkibwa wa maendeleo ,hivyo kuwataka wanawake kuwa mstari wa mbele katika kupiga vita rushwa  ili kupatikana kwa usawa katika  upatikanaji wa mikopo kwa wanawake ambapo pia ameishukuru serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kupigana vilivyo na tatizo la rushwa hapa nchini.

Pia ameshukuru kuwa dunia inatambua umuhimu wa kusaidia wanawake ili wanawake waweze kujikomboa kiuchumi pamoja na haya pia ameshukuru mabenki ambayo yametambua umuhimu wa kuwasaidia wanawake kwa kuwapa mikopo.


Katika hayo pia amesema changamoto kubwa inayowakabili tasisi nyingi ni ukosefu wa matawi ya benk vijijini  kwani makampuni mengi ya kibenki yamejiwekeza zaidi katika  miji mikubwa na kusau kujiwekeza vijijini na kutoa wito kwa makampuni ya  kibenki kushirikiana na Taasisi ya Selfina katika  kutoa mikopo ya bei nafuu kwa wana wake ili kuweza kuwasaidia wananwake wa mjini na vijijini kuinuka katika suala la kimaendeleo na kiuchumi.  

No comments:

Post a Comment