Thursday, July 4, 2013

MFANYABIASHARA AWAGONGA WATU SITA KATIKA UGOMVI WA KUMGOMBEA MWANAMKE KWA KUTUMIA GARI

 
Kamishna wa polisi kanda maalum Dar es salaam Suleiman Kova

Jeshi la polisi kanda maalaum Dar es salaam linamshikilia mfanyabishara mmoja kwa tuhuma za kuwagonga  na gari kwa makusudi watu sita  na kuwasababishia  majereha huku mmoja akiwa mahututi kwa sababu ya wivu wa mapenzi.

Akielezea tukio hilo la aina yake kamishana wa polisi kanda maalum suleiman kova amesema tukio hilo lilitokea katika eneo la bahari beach kwenye baa iitwayotwayo Kilongawima resort wakati alipokuwa na rafiki wake wa kike.

Kamishna amesema bwana Heven akiwa na rafiki yake huyo wa kike aliyetambulika kwa jina la Jovita alihama meza na kuhamia katika meza ya jirani walipokuwa wamekaa wanaume sita na alipojaribu kumuita wanaume hao walimcheka na kumdhihaki bwana heven.

Bwana Heven kuona anadhaulika alichukua gari yake yenye namba za usajili T 546 BXX aina toyota hilux na kuwagonga watu hao sita na kuwasababishia majerha na mmoja kulazwa akiwa mahututi huku msichana jovita akitokomea pasipo julikana na mtuhumiwa baada ya tukio hilo alijaribu kujiua lakini alizuiliwa


walipata mkasa huo wa kugongwa na bwana Heven Mmari ni Solomon kirato,Peter Marwa,Yahaya Albert ,Noah Mmari na wengine ambao hawajajulina  na wamelezwa katika hosptali ya Moi baada ya kupata majeraha ya kuvinjika vunjika na wengine kuumia sehemu za kichwana.

wakati huo huo jeshi lapolisi  kanda maalum  linawashikilia majambazi watatu baada kukamatwa huko ilala wakiwa wakiwa na bastola aina ya Bereta  ikiwa na risasi nane kwenye magazine na risasi zingine tano wakiwa wameficha kwenye pakiti  ya sigara ,watuhumiwa hao ni Emmanuel Muya miaka 30 mkazi wa Mbagala ,Ahamed Abdalah miaka 20 mkazi wa karata ,Jasmini Rajabu au Asha ambaye ni mama Lishe na mkazi wa Mbagala.

Watuhumiwa hawa pia wamekamatwa na pikipiki aina ya boxer T 836 CLA .

Wakati majambazi hao wakikamatwa jeshi hilo pia limefanikiwa kukamata malighaf bandia za kutengenezea pombe kali aina ya konyagi .

Tukio hilo limetokea mnamo tarehe 28/6/2013 huko wilaya yaTemeke Yombo Buza mtaa wa capetown ambapo polisi walikamata mtuhimiwa January Kimaro mfanyabiashara na mkazi wa Buza capetown akiwa na pakiti tupu zipatazo 50 za konyagi ,chupa tupu za konyagi 10 na spirit lita 10 ikiwa ni vifaa vya kutengeneza pombe haramu bandia aina ya konyagi ,mtuhumiwa anaendelea kushikiliwa na kuhojiwa.


Katika tukio lingine kamishana Suleiman Kova amesema jeshi hilo limewafanikiwa kuwakamata watuhumiwa 28 kwa tuhuma za kukutwa na pombe haramu ya Gongo lita 100  huko katika maeneo ya Mchambawima,mkwajuni,kigogo mwembe jando na kigogo mwembe sindano maeneo haya yote yapo katika wilaya ya kinondoni katika jiji la Dar es slaam na watuhumiwa waliokatwa ni Ally Shomari ,Mohameds Ahamed na watuhumiwa wengine 26 ambao wote watapelekwa mahakamani upelezi utakapo kamilika.


Kamishina wa polisi kanda maaluma amemaliza kwa kuwashukuru wananchi wote,jeshi la ulinzi la wananchi Tanzania ,idara ya usalama wa Taifa  ,wanahabari  kwa kufanikisha kuimarisha ulinzi wakati wa ujio wa marais wa nchi 14 na wake zao pamoja na wakati wa ujio na kuondoka kwa rais wa marekani Barack obama kwani hawakuona mabango wala vipeperushi  au maandamo ya  kupinga ujio wa Rais wa Marekani Barack Obama.

No comments:

Post a Comment