Wednesday, March 26, 2014

Matukio mbalimbali katika picha Bungeni leo mjini Dodoma

Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, akizungumza na waandishi wa habari, kuelezea msimamo wa umoja wao wa Ukawa, pamoja na mambo mengine lakini kuhusu uamuzi uliofanywa na Mwenyekiti wa bunge hilo, Samuel Sitta, kuteua wajumbe wengi kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuingia katika Kamati ya uongozi na kuchagua mmoja tu katika upande wa Vyama vya Upinzani, nje ya ukumbi wa Bunge, mjini Dodoma usiku wa kuamkia leo.
Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza (kulia) na Hezekiah Chibulunje, wakizungumza jambo wakati wakielekea kwenye ukumbi wa Bunge kwa ajili ya kikao cha asubuhi, mjini Dodoma leo. 
Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, viongozi wa Umoja wa Utetezi wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba na wa Chadema, Freeman Mbowe, wakijadili jambo wakati walipokuwa wakitoka kwenye kikao chao cha umoja huo leo asubuhi kwenye ukumbi wa Bunge wa Msekwa, mjini Dodoma.
Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, viongozi wa Umoja wa Utetezi wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba na wa Chadema, Freeman Mbowe, wakijadili jambo wakati walipokuwa wakitoka kwenye kikao chao cha umoja huo leo asubuhi kwenye ukumbi wa Bunge wa Msekwa, mjini Dodoma.

Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Mussa Zungu (kushoto), akimuonesha kitu kwenye simu, mjumbe mwenzake, Kingunge Ngombale Mwiru, wakati walipokuwa wakibadilishana mawazo nje ya ukumbi wa Bunge, mjini Dodoma leo.
Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, wakibadilishana mawazo ndani ya ukumbi wa Bunge, mara baada ya Mwenyekiti wa bunge hilo, Samuel Sitta kuliaghirisha mpaka jioni.
Baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kutoka CCM, wakibadilishana mawazo ndani ya ukumbi wa Bunge, mara baada ya Mwenyekiti wa bunge hilo, Samuel Sitta kuliaghirisha mpaka jioni.
Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, akiteta jambo na Mchungaji Ernest Kadiva (kushoto) na Askofu Donald Mtetemela (kulia), ndani ya ukumbi wa Bunge, mara baada ya Mwenyekiti wa bunge hilo, Samuel Sitta, kuliaghirisha mpaka jioni leo.

No comments:

Post a Comment