Monday, October 10, 2016

Mshukiwa wa ugaidi Al-Bakr azuiwa na polisi Ujerumani

Jaber al-Bakr
Baada ya kusakwa kwa siku mbili, Polisi Ujerumani imemkamata raia wa Syria anayeaminika kupanga shambulio la kijihadi.
Jaber al-Bakr, aliyewasili Ujerumani kama mkimbizi, alikamatwa kwenye nyumba moja mjini Leipzig Jumatatu alfajiri.
Aliomba usaidizi kutoka kwa raia mwengine wa Syria, aliyewaarifu polisi na kumfunga kwa kamba, taarifa zinasema.
Al-Bakr alianza kusakwa baada ya polisi kugundua vilipuzi katika nyumba aliyokuwa akiishi .
Katika uvamizi wa awali mjini Chemnitz mapema Jumamosi, al-Bakr, mwenye umri wa miaka 22, aliponyoka kukamatwa wakati maafisa walipofyetua risasi katika jaribio lililotibuka la kumkamata.
'Maabara ya vilipuzi'
Polisi iligunduwa vilipuzi na kilo ya kemikali katika nyumbani yake kwenye mji wa mashariki Chemnitz. Taarifa zinaashiria kemikali hiyo ni TATP, kemikali ya vilipuzi iliyotumiwa katika mashambulio ya kijihadi Paris na Brussels katika mwaka uliopita.
Duru za usalama zilitaja nyumba ya al-Bakr's kama 'maabara ya vilipuzi' na waliviharibu vilipuzi hivyo katika mlipuko uliodhibitiwa.

No comments:

Post a Comment