Thursday, May 31, 2012

RAIS KIKWETE AFUNGUA MKUTANO WA AFDB LEO ARUSHA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akifungua mkutano wa 47 wa mwaka wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB)
 Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Ivory Cost Dr. Alassane Ouattara (kushoto) akibadilishana mawazo na Rais wa wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dr.Donald Kaberuka(kulia) wakati wa sherehe za ufunguzi wa  mkutano wa 47 wa mwaka wa Benki ya Maendeleo ya Afrika
 Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Ivory Cost Dr. Alassane Ouattara akihutubia wakati wa sherehe za ufunguzi wa  mkutano wa 47 wa mwaka wa Benki ya Maendeleo ya Afrika
 Rais wa wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dr.Donald Kaberuka akihutubia wakati wa sherehe za ufunguzi wa  mkutano wa 47 wa mwaka wa Benki ya Maendeleo ya Afrika
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Jakaya Mrisho Kikwete(kulia) akibadilishana mawazo na Waziri wa Fedha Dr. William Mgimwa (kushoto)  wakati wa sherehe za ufunguzi wa  mkutano wa 47 wa mwaka wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) 
 Baadhi ya wajumbe wa Mkutano wa 47 wa mwaka wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AFDB) wakifuatilia kwa makini hotuba ya Rais Kikwete wakati wa ufunguzi wa mkutano huo jana mjini Arusha
muonekano wa jengo la mikutano la AICC kwa mbele
Nchi  za Afrika  zinarasilimali nyingi lakini baadhi zimeshindwa kuendelea kutokana na kutokuwa na mfumo mzuri wa usimamizi wa rasilimali hizo ili kuondokana na tatizo la umaskini.

Hayo yalisemwa leo Jijini Arusha na Rais Jakaya Kikwete wakati alipokuwa akifunga mkutano wa mwaka wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB)ulioshirikisha wajumbe zaidi ya 2000 kutoka nchi mbalimbali za Bara la Afrika pamoja na Ulaya.

Alisema Afrika inafursa nzuri ya uwekezaji katika sekta ya utalii,kilimo,afya lakini baadhi ya nchi ndio zinanufaika na maendleo hayo kutokana na kusimamia rasilimali zao vizuri pamoja na kuwa na mifumo bora ya utawala pamoja na usimamia wa sheria.

Alisema  nchi za kiafrika zinakabiliwa na changamoto kubwa  katika kukuza uchumi wake kwa sababu ya hali ya kiuchumi ya kidunia sambamba na swala la chakula pamoja na upandaji wa bei ya mafuta hivyo kupelekea  ukuaji wa uchumi  kusuasua.

Alisema  sambamba na changamaoto hiyo pia tatizo la teknolojia  ndio linazozirudisha nyuma nchi za kiafrika kwa maana teknilojia kubwa ambazo nchi za kiafrika zinategeamea nyingi zinatoka nchi za nje.

Aidha raisi Kikwete ametoa rai kwa nchi za kiafrika katika kuondokana na changamoto hizo ambazo zinarudisha nyuma uchumi wa Afrika badala yake aliwasihi waafrika   kuchangamkia fursa zilizopo katika nchi zao
ambazo wakizitumia ipasavyo  uhakika wa maendeleo utakuwepo.

Miongoni mwa fursa zilizopo Afrika ni pamoja na rasilimali za utalii endapo kama watatumia rsilimali ya utalii ambapo zaidi ya nusu ya watalii duniani hufanya utalii wao katika nchi za kiafrika na kuingiza pato kubwa kwa taifa .
Sambamba na kuangalia sekta hiyo ya utalii pia Kikwee  alisema  kuna umuhimu mkubwa sana wa nchi za kiafrika kuangalia na kuweka mazingira mazuri  ambayo yatawavuti watalii kwa wingi ikiwemo kuweka miundombinu
bora ya Barabara, Viwanja vya ndege pamoja na bandari zetu.

Aliongeza kuwa endapo  mazingira ya miundo mbinu yataboreshwa sekta ya utalii  Barani Afrika itaingiza pato kubwa akitolea mfano nchi ya Tanzania kwa kusema kuwa kwa sasa pato kubwa linatoka katika madini na

huku utalii ikiwa inashika nafasi ya pili kwa kuingiza pato kubwa.

Faida ambayo nchi za kiafrika zitaiata kwa kukuza utalii ni kubwa kwa sababu katika sekta hii watalii wanapokuja huleta mafanikio ndani ya nchi husika tofauti na sekta ya madini ambapo wanaochimba huja kuchimaba na kuondoka nayo madini.


Naye Rais wa Benki ya AfDB,Dk, Donald Kaberuka Alisema AfDB inatoa misaada kwa nchi mbalimbali na kusisitiza kuwa misaada hiyo ilenge kuwasaidia wahusika pamoja na kuziinua taasisi ndogo ambazo zinahitaji misaada ya kifedha kwaajili ya kuendelea biashara zao pamoja na kutoa angalizo kwa Afrika kusimamia haki, sheria na utawala bora ili kila nchi iweze kunufaika na rasilimali zake.


Naye Rais wa Ivory  Cost,  Alassane Ouattara  alisema nchi hiyo ilikumbwa na machafuko ya kisiasa lakini hivi sasa hali ya serikali imejitahidi kumaliza suala hiyo na amani imerudi tena.

Alisema serikali  imejipanga kuhakikisha uchumi wan chi hiyo unakuwa na katika kudhibitisha hilo serikali hiyo Juni mwaka huu hadi 2015 inatarajia kuzindua mpango mkakati wa kukuza uchumi katika nchi hiyo ili kila mwananchi aweze kunufaika na kile anachozalisha.

No comments:

Post a Comment