Friday, June 1, 2012

Mkutano wa Somalia waendelea Uturuki


Mkutano wa Kimataifa kuhusu Somalia uliendelea kwa siku ya pili Ijumaa Mjini Instanbul, Uturuki kujadili changamoto za kisiasa na kiuchumi zinazoikabili nchini hiyo ikiwa ni pamoja na muda wa mwisho wa serikali ya mpito. 

Waziri Mkuu wa Somalia, Abdiweli Mohammed ameelezea matumaini ya nchi yake kuondoka katika hali mbaya iliyomo hivi sasa na kuwa na mchango muhimu kwa jumuiya ya kimataifa.

Katika taarifa yake iliyojaa matumaini aliyoisoma mbele ya mamia ya Wasomali na wajumbe kutoka kona mbalimbali duniani waliohudhuria mkutano huo, Waziri Mkuu huyo alisema Somalia ina mambo mengi mazuri kuliko uharamia, wanamgambo na njaa, na kuongeza kuwa Wasomali wanaweza kuifundisha dunia mambo kadhaa kuhusu uthabiti.

No comments:

Post a Comment