Thursday, June 14, 2012

ofisin kwa mkuu wa wilaya
habari na pual joseph manyara
 
Wananchi wa Wilaya ya Mbulu wameandamana hadi katika ofisi ya Mkuu wa wilaya kupinga kitendo cha kufungwa kwa ofisi ya serekali na kiongozi kufanya shughuli ya kuendesha pikipiki maarufu kama boda boda badala ya kuhudumia wananchi kama alivyo agizwa na serekali.

Wakiongea kwa jazba mbele ya Mkuu wa wilaya Bw Anator Choya wananchi wamebainisha kuwa ofisa mtendaji wa kata Ayamamii Bw Ibrahimu Tsere amekuwa amekuwa akifunga ofisi ya kijiji hivyo kuwawiya vigumu kupata huduma za serekali na kila wanapojaribu kumuuliza kuhusu swala hilo amekuwa akiwatolea vitisho.

Mkuu wa wilaya Bw Choya aliagiza mtendaji huyo afikishwe mara moja kwenye ofisi ya wilaya ili aeleze sababu ya kufunga ofisi na kufanya mambo ambayo ayahusiani na kazi ya serekali kwani kuendesha boda boda ni shughuli yake binafsi isiyo na manufaa kwa wananchi, `Kesho asubuhi naomba mkurugenzi wa halmashauri ya Mbulu aje na mtendaji huyo hapa ofisini ili atueleze kazi aliyo tumwa na serekali laasivyo pikipiki yake tutaichukuwa na kama asipo kuja kwa hiyari polisi watamchukuwa wamlete hapa` alisema Bw Choya.

Aidha mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mbulu Bw Simoni Mayeye alisema kwa upande wa wananchi ni halali kupata huduma za afisa mtendaji na hata atua waliochukua ni sawa kwani hili ni swala la msingi kwa wananchi` Maandamano haya ni ushahidi tosha kuhusu kufungwa kwa ofisi na mtendaji huyo na sisi tumesha toa maagizo kuwa ofisi za serekali zifanye kazi kwa muda wote na hapa lazima hatua za kinizamu zichkuliwe juu ya mtendaji huyo` Alisema Bw Mayeye

Wananchi walimchagua Bw John Darabe kuwa katibu wa kata katika kikao kilicho amriwa na mkuu wa wilaya kufanyika kwa lengo la kutatua tatizo la uongozi wa kijiji hicho mkutano ambao mkuu wa wilaya amewaahidi wananchi kuwa kero zao zote zitasikilizwa na kutatuliwa.

Mmoja kati ya wananchi hao Bw Israeli Bilauri alibainisha kuwa wamekuwa wakinyanyasika na vitisho vya mtendaji huyo na wamekuwa wakikosa huduma za serekali, `Ofisi hii imekuwa ikifunguliwa siku anayo take yeye mwenyewe na tulipo jaribu uliza alitujubu kuwa sisi hatuku mwajiri yeye nay eye ndinye mwenye maamunzi` alisema Bilauri.

Vitendo vya viongozi wa serekali za vijiji na kata kuwazarau na kuwapuuzia wananchi vimekuwa vikijitokeza hasa katika maeneo ya vijijini na kuwakosesha wananchi haki zao za msingi kwani viongozi hawa wamekuwa kama wafalme katika jamii kwani hata wakifanya maamuzi wanafanya kwa manufaa yao binafsi na wananchi hawana cha kufanya Bwana Israel Bilauri aliweka wazi kuwa Mzee Margwe Masang kuchukuliwa dume la ng`ombe na uongozi wa kijiji kwa kushindwa kutoa mchango wa elfu sitini na tano (65) na wamekuwa wakimzungusha Mzee huyo mapaka leo ` Huyo ni Mzee na imewekwa wazi kuwa wazee hawatakiwi kuchangia lakini kwanini mambo haya lakini kwanini wamemchukulia dume la ng`ombe na sasa kumlipa mzee huyo ng`ombe wake uongozi unamzungusha tuu mpaka leo` alisema Bilauri



Wakati huo huo Mwanafunzi wa shule ya sekondari Genda wilayani Mbulu mkoani Manyara ( 20) amanusurika kubakwa na watu wawili wakati akitoka katika masomo ya jioni.

Pascalina ameeleza kuwa akiwa anatoka kujisomea darasani alikutana na watu wawili wakamwomba awaonyeshe njia na ndipo alipo sogea karibu wakamshika na kumpeleka katika uwanja wa mpira Sanu na kumuekea nguo mdomoni na kuanza jaribio la kumbaka lakini alijitahidi kupambana na wabakaji na alifanikiwa kutoroka kutoka katika mikono ya wabakaji hao

Vitendo vya ubakaji kwa sasa vimeshamiri katika mkoa wa manyara na jamii inekuwa ikihofia kutoa taarifa kwa jeshi la polisi kwa kuhofia kutoa ushahidi mahakamani kwani mara tuu baada ya jaribiao hilo wahalifu hao walikimbila kusiko julikana Mlezi wa Pascalina Bi Maria Naasa alisema kuwa `Ningumu kwa sasa kupeleka swala hili polisi kwani Pascalina ni mgeni hapa na hata wahalifu hao hawajui akiwaona sasa kweli swala hili utawaambiaje polisi nay eye hawajui wabakaji`

Wakazi wa Sanu wameeleza kuwa matukio ya ubakaji na wizi yameshamiri kwa kasi katika maeneo yao na hasa katika eneo la Uwanja wa Mpira kwani hili ni moja tuu kati ya matukio mengi yanayo tokea eneohilo na jamii imekaa kimya kwani kumesha wahi kutokea ubakaji mwingine katika eneo hili.

Bwana Herman Kita ni mkazi wa Sanu alibainisha kuwa waalifu wanaotenda vitendi hivyo wanajulikana, ` Wabakaji wanajulikana tatizo ni wazazi wao ni watu wenye pesa sasa na wamekuwa wakifanya ubakaji katika eneo la uwanja wa mpira lakina hakuana cha kuwafanya wazaziwao wanauwezo kipesa sasa kila siku unasikia binti wa flani kabakwa na watoto wa mzee flani sasa hatuna chakufanya na hata kama tukienda polisi kesho wanatoka` —

No comments:

Post a Comment