Tuesday, June 12, 2012

POLISI WAKAMATA LITA 9000 ZA GONGO

JESHI la polisi mkoani hapa limefanikiwa kukamata pombe lita 9000 ya pombe  haramu  aina ya gongo iliyokuwa ikisafirishwa kutoka nchini Kenya kuingia nchini Tanzania.

Kamanda wa polisi mkoani hapa, ACP Liberatus Sabas alisema kuwa tukio hilo limetokea juni 10 mwaka huu majira ya saa 12;00 jioni katika eneo la Namanga wilayani Longido, ambapo askari wa jeshi la polisi mkoani Arusha walifanikiwa kumkamata mtu mmoja aitwaye Nicolaus Thobias (35) mkazi wa Arusha mjini.

Alisema kuwa ,dereva huyo alikuwa amehifadhi pombe hiyo kwenye pipa 150 ambapo polisi walifanikiwa kukamata baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema .

Sabas alisema kuwa, dereva huyo alikuwa amebeba pombe hiyo kwenye gari aina ya Scania lenye namba za usajili T 416 AJX ambalo linamilikiwa na Joseph Michael Massawe.

 Awali baada ya kumkamata mtuhumiwa huyo, alisema kuwa anasafirisha spirit lakini mara baada ya upekuzi ikagundulika kuwa ni pombe  haramu ya gongo.

Kamanda Sabas aliongeza kuwa, kufuatia tukio hilo jeshi la polisi linaendelea kumshikilia dereva huyo kwa mahojiano zaidi na pindi uchunguzi utakapokamilika atafikishwa mahakamani kujibu shitaka hiyo.

No comments:

Post a Comment