Tuesday, June 12, 2012

WAMILIKI WA MADUKA YA MADAWA BARIDI WAONYWA KUTONUNUA DAWA KWENYE HOSPITALI ZA SEREKALI

WAMILIKI wa Maduka ya dawa baridi, wametahadhrishwa kutokuchukua dawa katika hospital za serikali na kuzipeleka kenye maduka yao  kwa ajili ya biashara huku hospital zikiwa hazina dawa kwa ajili ya wagonjwa.

Hayo yameelezwa jana na mganga mkuu wa mkoa wa Arusha, dakta Frida Mokiti, alipokuwa akifungua mafunzo ya wiki moja ya watoa dawa  katika maduka ya dawa muhimu, inayoshirikisha wauzaji wa dawa kutoka halamashauri ya Jiji la Arusha na wilaya ya Arusha DC,katika ukumbi wa chuo cha Ufundi, Arusha yaliyoandaliwa na mamlaka ya Chakula na dawa..
Dakta, Mokiti, alisema  kuwa kuna baadhi ya wamiliki wa maduka ya dawa ambao wamekuwa wakitumia ujanja kujipatia dawa hizo kutoka katika hosipital za serikalini na kuzipeleka kwenye maduka yao huku wagonjwa wakibakia bila dawa hivyo akawaonya kuacha tabia hiyo mara moja kwani msako utapita na atakaepatikana akiuza dawa hizo atakabiliwa na wakati mgumu.

Alisema lengo la serikali kutoa  mafunzo hayo kwa watoa dawa katika maduka ya dawa muhimu, ni ili kuwawezesha kupata elimu bora ya utoaji sahihi wa dawa na hivyo kuweza kuondoa tatizo huduma hafifu mkoani Arusha.

Alisema mafunzo hayo ambayo yanalenga katika sheria na kanuni zinazosimamia dawa sanjari na magonjwa yatokeayo mara kwa mara ,matibabu ya magonjwa  ya watoto kwa uwiano ,elimu ya ukimwi  na ushauri nasaha ,mbinu mbalimbali za mawasiliano  na elimu ya uzazi wa mpango.

Dakta mokiti, alisema kuwa  mafunzo hayo ni ya msingi na yatawasaidia  kuwa watoa huduma wazuri na kuimarisha utendaji wao ,na dawa zitatumika kwa usahihi  na kutoa matunda yaliyokusudiwa na madaktari ,pia wakumbuke kuwa dawa ni sumu iwapo hazitatumika  ilivyokusudiwa zinaweza kulata madhara  ambayo hayakutarajiwa kwa watumiaji.

Awali Meneja wa kanda ya kaskazini Damas Matiko, kutoka mamlaka ya Chakula na dawa TFDA ,alisema kuwa mamlaka imeaandaa mafunzo hayo kutokana na tathimini iliyofanywa mijini na vijijini,  na kubaini kuwepo kwa matatizoya upatikanaji wa huduma za msingi imeendelea kuwa ni tatizo  katika sekta hiyo ya dawa baridi hivyo mafunzo hayo yatasaidia kupata ufumbuzi wake.

Alisema katika tathimini hiyo matatizo yaliyojitokeza ni pamoja na watoaji  wa dawa katika  maduka kutokuwa na elimu  ya dawa au tiba ,kuuza dawa moto ambazo hazikusajiliwa kutoa huduma za tiba kwenye maduka sanjari na kuchoma sindano wagonjwa na ,kufunga vidonda .

Matiko,alisema kutokana na matatizo hayo serikali kupitia wizara ya afya na usitawi wa jamii  kwa kushirikiana na MSH ilibuni mpango wa majaribio, ADDO, ambao umetekelezwa katika mkoa wa Ruvuma kuanzia February 2002 hadi Julai 2005 .

Ameyataja mafanikio hayo kuwa ni pamoja na kuongezeka kwa upatikanaji wa dawa zenye ubora ,usalama na ufanisi, kuimarika kwa mfumo wa ukaguzi na usimamizi wa ,kuongezeka kwa ubora wa majengo na kiwango cha usafi wa majengo na watoa huduma, kuanzishwa na kuimarika kwa utunzaji wa nyaraka na kumbukumbu na staid za kazi kati ya wagonjwa na watoa huduma.

 Matiko,alisema kutokana na mafanikio hayo serikali imeamua kusambaza mpango huo nchi nzima ambapo umetekelezwa katika mikoa ya Ruvuma, Mtwara,Rukwa, Morogoro, Singida, pwani.lindi, mbeya,Kigoma, dodoma, Iringa, Mara, Tanga, na Manyara .

Mpango huo pia upo katika hatua ya kutekelezwa katika mikoa ya Shinyanga, Tabora, Kagera, Kilimanjaro, na kwenye makao ya kanda katika miji mikubwa ya Arusha, Mwanza  na dare s salaam,

Alisema mafanikio ya utekelezaji wa mpango huo yamepelekea nchi za Zambia na Uganda kuja nchini kujifunza  namna ya kuboresha utolewaji wa huduma hizo za dawa baridi katika maduka kwenye mataifa hay

No comments:

Post a Comment