Wednesday, August 15, 2012

Helikopta mbili za Uganda zapatikana

Mabaki ya helikopta iliyoanguka
Mabaki ya helikopta mbili za kijeshi za Uganda yamepatikana katika msitu wa Mlima Kenya. Helikopta hizo zilianguka katika eneo hilo zilipokuwa njiani kuelekea Somalia.\

"Helikopta zimepatikana lakini zimeungua kabisa," alieleza afisa mmoja wa jeshi la Kenya. "Hatufahamu hatma ya waliokuwa kwenye helikopta hizo." Msemaji wa jeshi la Kenya, Bogita Ongeri, amethibitihsa kupatikana kwa mabaki ya helikopta hizo. Juhudi za uokozi bado zinaendelea. Mpaka sasa hakuna taarifa zozote juu ya watu kumi waliosemekana kuwa ndani ya helikopta hizo za kijeshi.


Helikopta nyingine ya jeshi la Uganda, ilianguka Jumapili katika misitu ya Mlima Kenya lakini wanajeshi saba wa Uganda waliokuwa ndani ya helikopta hiyo waliweza kuokolewa. Helikopta zote tatu ni za aina ya Mi-24 na zimetengenezwa Urusi. Zilikuwa zikielekea Somalia kuungana na majeshi ya Umoja wa Afrika katika mapambano dhidi ya kundi la kigaidi la al-Shabaab. Helikopta nyingine ambayo ni aina ya Mi-17 ilianza safari Jumapili kuelekea Somalia na kutua salama mjini Garissa, Kenya, ambapo iliongeza mafuta kabla ya kuendelea na safari.


Mabaki ya Helikopta ya Uganda na waokoaji
Mabaki ya Helikopta mbili za Uganda ambazo ziliripotiwa kutoweka siku ya Jumapili zimepatikana mashambani nchini kenya.



No comments:

Post a Comment